logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mbappe na Vinícius Junior ni mingoni mwa wachezaji wanne wa Real Madrid wanaochunguzwa

Vyombo vya habari vya Uhispania vilisema kwamba Atletico Madrid iliripoti vitendo hivyo kwa Uefa wiki iliyopita.

image
na Japheth Nyongesa

Football28 March 2025 - 11:47

Muhtasari


  • Tukio hilo ambalo limeanza kufanyiwa uchunguzi lilifanyika wakati timu hiyo ya soka ikiwa ugenini kwa Atletico Madrid.
  • Katika taarifa, Uefa ilisema: "Mkaguzi wa maadili na nidhamu ameteuliwa kuchunguza madai ya mwenendo usiofaa" yaliyotolewa na wachezaji wanne wa Real Madrid.

Real Madrid Players
Ligii kuu ya mabingwa ulaya UEFA imeanzisha uchunguzi juu ya wachezaji wanne wa timu ya soka ya Real Madrid kutokana na jinsi walivyoshrehekea ushindi kwenye mechi yao ya raundi ya 16.

Wachezaji hao ambao wako chini ya uchunguzi wanajumuisha washambuliaji wawili Kylian Mvbappe na Vinicius Junior. Wengine ni pamoja na Dani Caballos na mlinzi Antionio Rudiger.

Tukio hilo ambalo limeanza kufanyiwa uchunguzi lilifanyika wakati timu hiyo ya soka ikiwa ugenini kwa Atletico Madrid.

Wachezaji hao wanne wanadaiwa kufanya ishara kwa mashabiki wa nyumbani baada ya Real Madrid kuwashinda wapinzani wao wa jiji kwa mikwaju ya penalti na kujikatia tiketi yao katika robo fainali.

Picha za televisheni zilionyesha beki wa Ujerumani Rudiger akionekana kufanya ishaya ya kukata koo, inaonekana kuelekea umati baada ya ushindi wa mikwaju, huku Mbappe akionekana kufanya ishara ya kunyakua gongo. 'gesture'

Vyombo vya habari vya Uhispania vilisema kwamba Atletico Madrid iliripoti vitendo hivyo kwa Uefa wiki iliyopita.

Wachezaji hao iwapo watapatikana na hatia wanaweza kuwa katika hatari ya kusimamishwa kucheza kwenye mechi kadhaa lakini hakuna hakikisho kwamba kesi hiyo itasikilizwa kabla ya robo fainali yao na Arsenal.

Mkondo wa kwanza wa mechi hiyo itafanyika kwenye Uwanja wa Emirates mnamo 8 Aprili na mkondo wa marudiano wiki moja baadaye.

Katika taarifa, Uefa ilisema: "Mkaguzi wa maadili na nidhamu ameteuliwa kuchunguza madai ya mwenendo usiofaa" yaliyotolewa na wachezaji wanne wa Real Madrid.

UEFA itachunguza ikiwa ishara za wachezaji hao zililenga moja kwa moja mashabiki wapinzani na ikiwa ni ukiukaji wa Kanuni za nidhamu. Ikiwa watapatikana na hatia ya kukiuka sheria, klabu na wachezaji wanaweza kukabiliwa na vikwazo.

 Real Madrid watalazimika kuwatetea wachezaji wake mbele ya UEFA, wakitoa ushahidi wa kuhalalisha tabia zao na kuepuka adhabu zinazoweza kutokea.

Klabu hiyo inasema kuwa sherehe hiyo ilikuwa ya hiari, ikionyesha tu mvutano wa mechi, na haikukusudiwa kuwachokoza wafuasi wa Atlético de Madrid.






RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved