logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Arne Slot azungumzia msitakabali wa Alexander Arnold na Salah kwenye timu ya Liverpool

Meneja wa Liverpool Arne Slot amesisitiza kwamba umakini wake unabaki kwenye matukio ya uwanjani

image
na Japheth Nyongesa

Football02 April 2025 - 13:55

Muhtasari


  • kini bosi huyo amesisitiza kwamba vipaumbele vyake vinabaki katika kuiongoza timu hiyo kwenye matokeo uwanjani
  • Na kumsaidia Alexander-Arnold kupona jeraha alilopata dhidi ya Paris Saint-Germain kabla ya mapumziko ya kimataifa.

Mohamed Salah and Alexander Arnold
Meneja wa Liverpool Arne Slot amesisitiza kwamba umakini wake unabaki  kwenye matukio ya uwanjani kufuatia habari za madai ya Trent Alexander-Arnold kujiunga na Real Madrid kwa uhamisho wa bure msimu wa joto.

Iliripotiwa mwishoni mwa mwezi uliopita kwamba Alexander-Arnold, ambaye mkataba wake unaisha mwishoni mwa msimu, alikuwa amekubaliana na wapenzi wake wa muda mrefu Real Madrid kuondoka katika klabu yake ya utotoni na kujiunga nao.

Habari hizo zinakuja kama pigo kwa kikosi cha Slot, lakini bosi huyo amesisitiza kwamba vipaumbele vyake vinabaki katika kuiongoza timu hiyo kwenye matokeo uwanjani na kumsaidia Alexander-Arnold kupona jeraha alilopata dhidi ya Paris Saint-Germain kabla ya mapumziko ya kimataifa.

"Hali yake kwa bahati mbaya ni kwamba amejeruhiwa," Slot alisema. "Vinginevyo watu wangesema kwamba alikuwa na onyesho moja au mbili nzuri kwa timu ya England.

"Lakini amejeruhiwa na kwake hiyo inamaanisha kuwa amezingatia kikamilifu kupona kwake. Kwetu sisi inamaanisha tutajaribu kumsaidia kurudi haraka iwezekanavyo," alieleza mkufunzi huyo.

Kocha huyo pia aliongeza kwamba kumekuwepo na mambo mengi ya kuwahusu Alexander Arnold, Van Dijk na Mo Salah ila wao kama viongozi wa timu hawajazingatia sana mazungumzo hayo.

"Na kwa wengine, kwa miezi minane iliyopita kumekuwa na maneno  juu na chini na mazungumzo juu ya Virgil van Dijk na Mo Salah, lakini hatujawahi kuzingatia mazungumzo hayo. Daima tumekuwa tukizingatia kile tunachopaswa kufanya," aleleza.

"Ni hali ambayo iko kwa miezi minane au tisa sasa na nadhani wachezaji hawa wote watatu wamefanya vizuri sana chini ya hali hizi kwa hivyo hainiathiri hata kidogo." aliongeza.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved