logo

NOW ON AIR

Listen in Live

EURO 2020: Mount na Chilwell watengwa na kikosi cha Uingereza

Wawili hao walitangamana na mchezaji Billy Gilmour wa Uskoti ambaye alipatikana kuwa na virusi vya Korona.

image
na Radio Jambo

Yanayojiri22 June 2021 - 03:44

Muhtasari


•Kulingana na ujumbe uliotolewa na timu ya Three Lions, wawili hao wametengwa kama tahadhari baada  ya mashauriano na kitengo cha afya ya umma Uingereza.

•Gilmour ambaye alichezea Uskoti mechi kamili yake ya kwanza Ijumaa lipimwa kuwa na maradhi ya COVID 19 siku ya Jumapili na atajitenga kwa kipindi cha siku kumi.

Ben Cilwell, Billy Gilmour na Mason Mount katika mechi ya Uingereza dhidi ya Uskoti Ijumaa

Wachezaji wawili wa timu ya taifa ya Uingereza almaarufu kama 'Three Lion' wametengwa kufuatia kutangamana na mchezaji Billy Gilmour wa Uskoti ambaye alipatikana kuwa na virusi vya Korona.

Ben Chilwell na Mason Mount ambao wanachezea klabu ya Chelsea wanadaiwa kutangamana na  mwenzao Gilmour kwenye mechi kati ya Uingereza na Uskoti usiku wa Ijumaa. Mechi hiyo iliisha sare tasa.

Kulingana na ujumbe uliotolewa na timu ya Three Lions, wawili hao wametengwa kama tahadhari baada  ya mashauriano na kitengo cha afya ya umma Uingereza.

Gilmour ambaye alichezea Uskoti mechi kamili yake ya kwanza Ijumaa lipimwa kuwa na maradhi ya COVID 19 siku ya Jumapili na atajitenga kwa kipindi cha siku kumi.

 Mount na Chilwell hawatatangamana na kikosi hicho kingine wakisubiria maamuzi ya afya ya umma. 

Wawili hao watakosa mechi dhidi ya Ucheki usiku wa leo.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved