logo

NOW ON AIR

Listen in Live

"Tupatane nje ya uwanja" Mshambulizi Allan Wanga atangaza kustaafu kwake baada kucheza soka miaka 14

Wanga amechezea klabu nyingi nchini ikiwemo Lolwe FC, Sher Karuturi, Tusker, AFC Leopards na Kakamega Homeboyz ilhali kimataifa amechezea Petro Atletico ya Angola, FC Baku ya Azerbaijani, Al- Merrikh ya Sudan, Hoang Anh Gia Lai ya Vietnam na Azam ya Tanzania.

image
na Radio Jambo

Habari12 September 2021 - 06:16

Muhtasari


•Wanga 35, ambaye ameshirikishwa kwenye timu ya Harambee Stars kutoka mwaka wa 2007 alitangaza kustaafu kwake kupitia kurasa zake za mitandao ya kijamii.

•Wanga amechezea klabu nyingi nchini ikiwemo Lolwe FC, Sher Karuturi, Tusker, AFC Leopards na Kakamega Homeboyz. Kimataifa Wanga amechezea Petro Atletico ya Angola, FC Baku ya Azerbaijani, Al- Merrikh ya Sudan, Hoang Anh Gia Lai ya Vietnam na Azam ya Tanzania.

Mshambulizi matata wa timu ya taifa na klabu ya Kakamega Homeboyz Allan Wetende Wanga ametangaza kustaafu kwake baada ya kucheza soka ya kitaalamu kwa kipindi cha miaka 14.

Wanga 35, ambaye ameshirikishwa kwenye timu ya Harambee Stars kutoka mwaka wa 2007 alitangaza kustaafu kwake kupitia kurasa zake za mitandao ya kijamii.

Mchezaji huyo amesema kuwa soka imempeleka mahali kwingi duniani ambako hakuwahi fikiria angewahi kufika.

Amesema kwamba amefurahia kipindi cha miaka 14 ambacho amekuwa akichezea timu ya taifa na klabu mbalimbali na kuwashukuru sana mashabiki ambao wamekuwa wakimtia motisha wa kucheza vyema zaidi.

"Miaka 14 nikifanya kitu ambacho kinakuleta raha, kuridhika na fahari  ni baraka. Nimekuwa nikiishi kwa hii baraka tangu nicheze kandanda kwa mara ya kwanza nikiwa mtoto mdogo na nikaanza kucheza soka ya kitaalam.

Mapenzi yangu kwa soka imenipeleka mahali ambako sikuwahi dhania ningewahi fika nikiwa na timu ya taifa na klabu. Nimeshuhudia ushindi na kupoteza, nimeinua vikombe, nimevumilia uchungu wa kukosa ushindi licha ya kuwa karibu nao, nimepitia yote.

Nimekuwa nikipewa msukumo na mapenzi pamoja na kuungwa mkono na mashabiki. Bila nyinyi mashabiki, wachezaji wenzangu, familia na wasaidizi katika klabu zote ambazo nimechezea singekuwa na motisha wa kuendelea mbele.Tafadhali pokeeni shukran zangu kwa yote, mliniinua wakati nilihitaji kuboresha mchezo wangu.

Ninapostaafu ningependa kuchukua fursa hii kuwapa shukran zangu. Nilikuwa hapo kwa kuwa mlikuwa na mimi. Shukran na Mungu awabariki. Tupatane nje ya uwanja." Wanga aliandika kwenye ukurasa wake wa Faceboook.

Wanga amechezea klabu nyingi nchini ikiwemo Lolwe FC, Sher Karuturi, Tusker, AFC Leopards na Kakamega Homeboyz. Kimataifa Wanga amechezea Petro Atletico ya Angola, FC Baku ya Azerbaijani, Al- Merrikh ya Sudan, Hoang Anh Gia Lai ya Vietnam na Azam ya Tanzania.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved