logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Kesi ya ubakaji dhidi ya Cristiano Ronaldo lazima itupiliwe mbali - Jaji

Ronaldo amekuwa wakati wote akikana kufanya kosa lolote.

image
na Radio Jambo

Habari09 October 2021 - 04:38

Muhtasari


•Waendesha mashitaka walichagua kutowasilisha mashitaka ya uhalifu dhidi ya Ronaldo katika mwakawa  2019 wakisema kuwa madai hayo yanaweza kuwa "hayakuthibitishwa vya kutosha".

Jaji amependekeza kuwa kesi ya ubakaji dhidi ya mshambuliaji wa Manchester United Cristiano Ronaldo nchini Marekani itupwe nje ya mahakama.

Inadaiwa kuwa Ronaldo mwenye umri wa miaka 36 alimyanyasa Kimapenzi mwanamke katika hoteli moja eneo la Las vegas mwaka 2009.

Waendesha mashitaka walichagua kutowasilisha mashitaka ya uhalifu dhidi ya Ronaldo katika mwakawa  2019 wakisema kuwa madai hayo yanaweza kuwa "hayakuthibitishwa vya kutosha".

Kesi ya kiraia ilifuatia madai ya mwanamke huyo kudai fidia ya uharibifu. Ronaldo amekuwa wakati wote akikana kufanya kosa lolote.

Hakimu Daniel Albregts, ambaye alichunguza upya kesi hiyo kabla ya jaji mwingine kufanya uamuzi wa mwisho, anasema ushahidi wenye misingi ya mawasiliano yaliyovuja baina ya Ronaldo na mawakili wake kutoka katika data zilizovuja za soka haungepaswa kutumiwa katika kesi.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved