logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Aston Villa yampiga kalamu kocha Dean Smith kufuatia msururu wa matokeo hafifu

Mkurugenzi mtendaji wa Villa Christian Purslow amesema uamuzi huo uliafikiwa sasa ili kupatia kocha mpya atakayeteuliwa wakati tosha wa kufanya mabadiliko ya kuboresha klabu.

image
na Radio Jambo

Yanayojiri08 November 2021 - 04:45

Muhtasari


•Mkurugenzi mtendaji wa Villa Christian Purslow amesema uamuzi huo uliafikiwa sasa ili kupatia kocha mpya atakayeteuliwa wakati tosha wa kufanya mabadiliko ya kuboresha klabu.

•Villa imetangaza kwamba tayari wameanza juhudi za kusaka kocha atakayejaza nafasi iliyoachwa wazi na Smith.

Klabu za soka za bara Ulaya zimeendelea kuwatimua kazi makocha ambao wameonekana kulemewa na kazi zao.

Klabu iliyofuta kocha wake hivi karibuni ni Aston Villa ambayo ilitangaza kuondoka kwa kocha Dean Smith siku ya Jumapili.

Smith ambaye ameongoza Villa tangu mwezi Oktoba mwaka wa 2018 alifutwa kazi baada ya klabu hiyo kupoteza katika mechi zote tano za hivi karibuni.

Mara ya mwisho Villa iliandikisha ushindi ilikuwa Septemba 25 ambapo ilishinda 0-1 ugenini dhidi ya Manchester United.

Mechi ya mwisho ambayo Smith alisimamia ilichezwa usiku wa Ijumaa dhidi ya Southampton ambapo Villa ilipokea kichapo cha 1-0 ugenini.

Mkurugenzi mtendaji wa Villa Christian Purslow amesema uamuzi huo uliafikiwa sasa ili kupatia kocha mpya atakayeteuliwa wakati tosha wa kufanya mabadiliko ya kuboresha klabu.

"Licha ya kuanza vizuri msimu uliopita, mwaka huu hatujaona uboreshaji endelevu wa matokeo, mwenendo na msimamo wa ligi ambao sote tumekuwa tukiutafuta. Kwa sababu hii tumeamua kufanya mabadiliko sasa ili kutoa muda kwa kocha mkuu mpya kufanya matokeo" Purslow alisema.

Villa imetangaza kwamba tayari wameanza juhudi za kusaka kocha atakayejaza nafasi iliyoachwa wazi na Smith.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved