logo

NOW ON AIR

Listen in Live

John Terry arejea Chelsea kama mshauri wa wachezaji wadogo

Chelsea imethibitisha kurejea kwa kiungo huyo wazamani zamani kwenye klabu hio, huku wakimpa mamlaka ya ushauri wa ukocha katika klabu hio

image
na

Burudani30 December 2021 - 05:18

Muhtasari


•Chelsea imethibitisha kurejea kwa kiungo huyo wa zamani katika klabu hio, huku wakimpa mamlaka ya ushauri wa ukocha katika klabu hio.

John Terry

John Terry, Beki wa zamani wa Uingereza , Jumatano aliwahakikishia mashabiki wa Chelsea   kurejea kwake kwenye timu hio.

Terry alionyesha furaha kubwa katika ukurasa wake wa Twitter akitangaza kurejea kurejea kwake katika uongozi wa wachezaji wadogo wa timu hio.

Chelsea imethibitisha kurejea kwa kiungo huyo wa zamani katika klabu hio, huku wakimpa mamlaka ya ushauri wa ukocha katika klabu hio.

Terry, ambaye ana umri wa miaka 41 alichezea Chelsea katika zaidi ya mechi 700 kama mchezaji na bado akiwa nahodha  na kusaidia timu hio kutoa mataji mengi

The Blues ilitangaza uteuzi wake kwa taarifa Jumatano, huku mchezaji huyo akitarajiwa kuanza kazi mara moja 

Beki huyo wa zamani wa Uingereza atachukua nafasi ya ushauri wa ukocha katika Akademi ya  Blues,  ambapo atakuwa akisaidia wachezaji wadogo pamoja na wakufunzi katika klabu hiyo ambapo alianzia tasnia yake ya kusakata kabumbu na kuibuka beki wa kusifika duniani

Jukumu la Terry katika klabu litahusisha kufundisha uwanjani, mijadala ya ukocha, ushauri wa wachezaji, pamoja na mazungumzo na wazazi. 

Uteuzi huu umegandia baada yake kuondoka Aston Villa  mapema mwaka.

 Terry alisaidia timu ya Chelsea kuibuka na kombe la primia Mara 5, tatu ikiwa chini ya Jose Mourinho, moja chini ya Carlo Ancelotti na moja chini ya Antonio Conte.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved