logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Lukaku awaomba msamaha mashabiki wa Chelsea

Lukaku ambaye alikosa Mechi ya Wikendi baina ya Chelsea na Liverpool, ambayo ilishia kwa sare ya kufungana 2-2. Alisema anajuta kwa maneno aliyoyasema kwenye kituo cha Sky  siku ya Jumatano

image
na

Makala05 January 2022 - 10:41

Muhtasari


•Lukaku amesema anajutia kwa maneno aliyoyasema kuhusu timu yake ya Chelsea na huku kuahidi kumakinika zaidi siku zijazo.

Mshambuliaji wa Chelsea Romelu Lukaku

Mchezaji wa Chelsea, Romelu Lukaku Jumanne alijitokeza wazi na kuomba msamaha mashabiki wa Chelsea kwa  Maneno aliyosema kuhusi ujio wake kwenye Klabu hio.

 Lukaku ambaye alikosa Mechi ya Wikendi baina ya Chelsea na Liverpool, ambayo ilishia sare ya kufungana 2-2. Alisema anajuta kwa maneno aliyoyasema kwenye kituo cha Sky  siku ya Jumatano

"Kwa mashabiki, samahani kwa usumbufu niliosababisha  Nyinyi mnajua uhusiano nilionao na klabu hii tangu ujana wangu, kwa hivyo ninaelewa kabisa hayo." Lukaku alisema kupitia mtandao wa Timu hio.

Aliendelea kuomba Kocha,Thomas Tuchel msamaha na kuhakikisha ako tayari kujituma kusaidia timu hio kufikia marengo yao ya msimu huu.

"Kwa meneja, naomba radhi, na pia kwa wachezaji wenzangu na bodi nisameheni , kwa sababu nadhani haikuwa wakati sahihi. pia ninataka kwenda mbele kutoka kwa hili jambo na kuhakikisha kuwa tunaanza kushinda michezo yetu"

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved