logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Cameroon yawashinikiza wafanyikazi kuhudhuria mechi za Afcon

Uamuzi huo umefikiwa baada ya michezo mingi kuchezwa katika mji wa Limbe kukiwa na mashabiki wachache.

image
na Radio Jambo

Makala18 January 2022 - 08:21

Muhtasari


•Uamuzi huo umefikiwa baada ya michezo mingi kuchezwa katika mji wa Limbe kukiwa na mashabiki wachache.

Wafanyakazi wa baraza huko Buea kusini-magharibi mwa Cameroon wanalazimishwa kuhudhuria michezo ya soka ya Kombe la Mataifa ya Afrika inayoendelea.

Hii inaambatana na maagizo ya gavana wa mkoa, kulingana na meya wa jiji, ya kutaka watu wote kuhudhuria kwa lazima michezo hiyo.

Uamuzi huo umefikiwa baada ya michezo mingi kuchezwa katika mji wa Limbe kukiwa na mashabiki wachache.

Buea ni mwenyeji wa timu zinazocheza huko Limbe.

Wakazi wengi wa Buea wanahofia makabiliano kati ya wapiganaji wanaotaka kujitenga na jeshi.

Wapinzani hao walioanza kupigana na serikali takriban miaka mitano iliyopita walikuwa wametishia kuvuruga mashindano hayo lakini serikali imewahakikishia usalama.

Miji kadhaa imetoa mabasi na magari kwa mashabiki wa soka ili kuongeza idadi yao viwanjani.

Serikali ya Cameroon siku ya Juma


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved