logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Tatizo la moyo lamlazimu Aubameyang kuondoka Afcon mapema

Raia huyo wa Gabon mwenye umri wa miaka 32 aliondoka katika kambi ya timu yake ya taifa siku ya Jumatatu na kurudi London ili kufanyiwa vipimo zaidi vya kiafya.

image
na Radio Jambo

Habari18 January 2022 - 04:46

Muhtasari


•Raia huyo wa Gabon mwenye umri wa miaka 32 aliondoka katika kambi ya timu yake ya taifa siku ya Jumatatu na kurudi London ili kufanyiwa vipimo zaidi vya kiafya.

Mshambulizi wa Arsenal na Gabon Pierre Emerick Aubameyang

Mshambulizi matata wa klabu ya Arsenal, Pierre Emerick Aubameyang amelazimika kukatiza safari yake ya AFCON baada ya kugunduliwa kuwa na vidonda vya moyo siku kadhaa tu baada ya kuugua Covid 19.

Raia huyo wa Gabon mwenye umri wa miaka 32 aliondoka katika kambi ya timu yake ya taifa siku ya Jumatatu na kurudi London ili kufanyiwa vipimo zaidi vya kiafya.

Shirikisho la soka la Gabon limethibitisha kwamba Aubameyang hatashirikishwa tena katika kikosi cha taifa hilo kwani tayari amepatiwa ruhusa kurudi Arsenal kwa masuala ya kiafya.

"Shirikisho la Soka la Gabon limeamua kuwarejesha wachezaji Pierre-Emerick Aubameyang na Mario Lemina katika vilabu vyao ili wafanyiwe mitihani zaidi ya afya" Shirikisho hilo lilisema katika taarifa fupi.

Aubameyang pamoja na mwenzake Mario Lemina wa Nice hawajashiriki katika mechi yoyote ya Afcon tangu kombe hilo lilipoanza baada ya kupatikana na virusi vya Corona siku chache kabla ya mechi ya kwanza ya Gabon.

Wawili hao wamekosa mechi mbili za Gabon ambapo timu hiyo imeandikisha sare ya 1-1 na ushindi wa 1-0 dhidi ya Ghana na Comoros mtawalia.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved