logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Shabiki sugu wa Simba ajitoa uhai siku ya mechi, aacha ujumbe azikwe na jezi ya klabu hiyo

Mnamo siku Khalfan alijitia kitanzi Simba ilipoteza 0-1 dhidi ya Mbeya City na wengi waliamini kwamba marehemu aliamua kujitoa uhai kutokana na mafadhaiko yaliyomkumba.

image
na Radio Jambo

Yanayojiri20 January 2022 - 03:13

Muhtasari


•Marehemu aliacha kama ameandika ujumbe kwa karatasi akiomba kuzikwa kama mwili wake umevalishwa jezi ya Simba  kutokana na upendo mkubwa aliokuwa nao kwa klabu hiyo.

•Mnamo siku Khalfan alijitia kitanzi Simba ilipoteza 0-1 dhidi ya Mbeya City na wengi waliamini kwamba marehemu aliamua kujitoa uhai kutokana na mafadhaiko 

Klabu ya soka ya Tanzania, Simba imeomboleza mmoja wa mashabiki wake sugu ambaye anaripotiwa kujitoa uhai mnamo Januari 17.

Khalfan Mwambena 17, ambaye alikuwa mkazi wa jiji la Mbeya alijitia kitanzi siku ya mechi kati ya Simba na Mbeya City FC.

Polisi jijini Mbeya wamethibitisha kwamba Mwambena alijitoa uhai kabla ya mechi hiyo wala si baada ya mechi hiyo kama ripoti za hapo awali zilivyokuwa zinadai.

Marehemu aliacha kama ameandika ujumbe kwa karatasi akiomba kuzikwa kama mwili wake umevalishwa jezi ya Simba  kutokana na upendo mkubwa aliokuwa nao kwa klabu hiyo.

"Naipenda sana Simba, I love you Simba na nikifa nizikwe na jezi ya Simba" Ujumbe ulioachwa na marehemu ulisoma.

Klabu ya Simba pamoja na mashabiki wamemuomboleza marehemu na kuitakia roho yake ilazwe mahali pema peponi.

"Khalfan ameonyesha mapenzi makubwa kwa Simba, Tunamuomba Mungu ailaze roho yake mahala pema peponi" Taarifa ya Simba inasoma.

Mnamo siku Khalfan alijitia kitanzi Simba ilipoteza 0-1 dhidi ya Mbeya City na wengi waliamini kwamba marehemu aliamua kujitoa uhai kutokana na mafadhaiko yaliyomkumba baada ya klabu aliyoipenda sana kupokea kichapo.

Hata hivyo Simba imepuuzilia mbali ripoti hizo.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved