logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Kiungo Mukangula ndiye mchezaji bora wa mwezi Desemba wa AFC Leopards

Kiungo wa kati wa timu ya AFC Leopards Eugine Mukangula ameibuka mchezxaji bora wa mwezi Disemba wa timu hiyo inayoshiriki ligi kuu ya soka nchini Kenya.

image
na Radio Jambo

Burudani01 February 2022 - 08:03

Muhtasari


Kiungo wa kati wa timu ya AFC Leopards Eugine Mukangula ameibuka mchezaji bora wa mwezi Disemba wa timu hiyo inayoshiriki ligi kuu ya soka nchini Kenya.

Kiungo wa kati wa timu ya AFC Leopards Eugine Mukangula ameibuka mchezaji bora wa mwezi Disemba wa timu hiyo inayoshiriki ligi kuu ya soka nchini Kenya.

Chingwe imetangaza haya Februari 1 na kusema kwamba katika kura zilizopigwa, Mukangula aliibuka mshindi huku akifuatiwa kwa ukaribu na wachezaji wenza Dan Musamali na Brian Wanyama.

Mukangula hadi sasa ndiye mfungaji bora wa timu ya AFC Leopards kwa mabao Matano, na amekuwa katika ubora wa kipekee uwanjani, huku akiisaidia Ingwe kupanda hadi nafasi ya kumi na mbili kwenye jedwali.

Kufuatilia ushindi huo, Mukangula anazawidiwa shilingi elfu 25 pamoja na kombe lililobinafsishwa kwa jina lake.

Kiungo huyo mahiri wa AFC Leopards pia anatarajiwa kuwania tuzo za mchezaji bora wa mwezi Januari baada ya kuwa na ustawi mkubwa kwenye mechi za Ingwe tangia mwaka wa 2022 kuanza.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved