logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Senegal yaingia fainali baada ya kuwalemea Burkina Faso

Timu ya taifa ya Senegal imejikatia tikiti katika fainali za AFCON 2022 baada ya kuwachabanga Burkina Faso mabao matatu kwa moja.

image
na Radio Jambo

Makala03 February 2022 - 04:25

Muhtasari


• Timu ya taifa ya Senegal imejikatia tikiti katika fainali za AFCON 2022 baada ya kuwachabanga Burkina Faso mabao matatu kwa moja.

• Hii imekuwa ni mara yao ya pili mtawalia kutinga katika fainali hizo baada ya kuibuka washinde katika kipute cha AFCON cha mwaka wa 2019 dhidi ya mbweha wa jangwani, Algeria.

Timu ya taifa ya Senegal imejikatia tikiti katika fainali za AFCON 2022 baada ya kuwachabanga Burkina Faso mabao matatu kwa moja.

Hii imekuwa ni mara yao ya pili mtawalia kutinga katika fainali hizo baada ya kuibuka washinde katika kipute cha AFCON cha mwaka wa 2019 dhidi ya mbweha wa jangwani, Algeria.

Senegal walifungua ukurasa wa magoli baada ya mpira wa kona kupigwa na kumkuta mkabaji wa kati wa timu ya Ufaransa PSG, Abdou Diallo aliyejinafasi vizuri katika kijisanduku na kuelekeza mpira wavuni baada ya dakika sitini na tisa za mchezo.

Bao la pili la Senegal lilifungwa na kiungo Idrissa Gueye baada ya mshambulizi matata Sadio Mane kummegea pasi nyeresi kunako dakika ya sabini na sita kabla ya Mane tena kufunga la tatu na kuwahakikishia Senegal nafasi katika fainali ya kipute hicho.

Timu ya Burkina Faso walipata bao la kifuta machozi kunako dakika ya 82 kutoka kwa mchezaji Toure.

Senegal sasa wanasubiria mshindi kati ya timu ya taifa ya Misri na wenyeji wa kipute cha AFCON, Cameroon. Fainali za kombe hilo zitachezwa Februari 6 katika uga wa Olembe jijini Yaounde.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved