Misri walifuzu kwa fainali ya Kombe la mabingwa barani Afrika (AFCON) baada ya kuwalaza wenyeji Cameroon katika nusu fainali iliyoishia kwa sare tasa muda wa kawaida.
Cameroon ambao wamekuwa na msururu wa matokeo mazuri waliondolewa kwenye michuano hiyo kupitia mikwaju ya penalti ambayo ilishia 3-1.
Misri, ambao ni mabingwa mara saba wa Afrika walianza michuano wakionekana kusuasua kwenye hatua ya makundi ila wakaendelea kuimarika hadi kufika fainali.
Kocha wa Misri, Carlos Queiroz alionyeshwa kadi nyekudu na sasa atakosa mchuano wa fainali ambayo itachezwa Jumapili dhidi ya Senegal.
Huu ulikuwa Mchezo wa kwanza kuchezewa uwanja wa Younde tangu mashabiki wanane kufariki kwenye lango la uwanja huo.
Fainali ya Jumapili itawakutanisha wachezaji wawili wa Livepool, Sadio Mane na Mohammed Sala.
Tunachosubiri ni kuona ni nani atanyakua kombe la mabingwa Afrika mwaka huu.