logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Misri yazamisha Cameroon kuingia fainali

Cameroon ambao wamekuwa na msururu wa matokeo mazuri waliondolewa kwenye michuano hiyo kupitia mikwaju ya penalti ambayo ilishia 3-1.

image
na

Burudani04 February 2022 - 04:24

Muhtasari


•Misri walifuzu kuingia fainali ya Kombe la mabingwa  Afrika(AFCON) baada ya kuwapiga wenyeji Cameroon kwenye nusu fanaila iliyoishia kwa sare muda wa kawaida.

•Misri, ambao ni mabingwa mara saba wa Afrika  walianza  michuano  wakionekana kuzuazua kwenye hatua ya makundi ila wakaendelea kuimarika hadi kufikia fainali.

wachezaji wa Misri wakisherekea kutinga fainali

Misri walifuzu kwa fainali ya Kombe la mabingwa  barani Afrika (AFCON) baada ya kuwalaza wenyeji Cameroon katika nusu fainali iliyoishia kwa sare tasa muda wa kawaida.

Cameroon ambao wamekuwa na msururu wa matokeo mazuri waliondolewa kwenye michuano hiyo kupitia mikwaju ya penalti ambayo ilishia 3-1.

Misri, ambao ni mabingwa mara saba wa Afrika  walianza  michuano  wakionekana kusuasua kwenye hatua ya makundi ila wakaendelea kuimarika hadi kufika fainali.

Kocha wa Misri, Carlos Queiroz alionyeshwa kadi nyekudu na sasa atakosa mchuano wa fainali ambayo itachezwa Jumapili dhidi ya Senegal.

Huu ulikuwa  Mchezo wa  kwanza kuchezewa  uwanja wa Younde tangu mashabiki wanane kufariki kwenye lango la uwanja huo.

Fainali ya Jumapili itawakutanisha wachezaji wawili wa Livepool, Sadio Mane na Mohammed Sala.

Tunachosubiri ni kuona ni nani atanyakua kombe la mabingwa Afrika mwaka huu.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved