logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Kocha wa Chelsea Thomas Tuchel asema 'si wakati wa kumkejeli' Lukaku

Amesema "hakuna wakati wa kumcheka"

image
na Radio Jambo

Makala22 February 2022 - 07:22

Muhtasari


•"Yuko kwenye uangalizi na tutamlinda. Romelu daima atakuwa sehemu ya suluhisho," Tuchel alisema

Mkufunzi wa Chelsea Thomas Tuchel amesema "hakuna wakati wa kumcheka" Romelu Lukaku baada ya mshambuliaji huyo aliyenunuliwa kwa kima cha takriban pauni milioni 97.5 kukabiliwa na changamoto uwanjani siku za hivi karibuni.

Lukaku alifanikiwa kugusa mpira mara saba tu katika mechi ya Jumamosi ambapo Chelsea ilipata ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Crystal Palace, kiwango ambacho ni cha chini kwa mchezaji yeyote kuwahi kugusa mpira katika dakika 90 za mechi ya Ligi ya Premia tangu mwaka 2003, wakati data hiyo iliporekodiwa mara ya kwanza.

"Yuko kwenye uangalizi na tutamlinda. Romelu daima atakuwa sehemu ya suluhisho," Tuchel alisema.

"Wakati mwingine inakuwa hivi kwa washambuliaji ikiwa wanajitahidi kidogo kujiamini na kutafuta nafasi ya kujihusisha na safu nzuri ya ulinzi.

"Bila shaka sio kile tunachotaka au anachotaka Lukaku lakini huu sio wakati wa kumcheka na kufanya masihara kumhusu."

Mshambuliaji huyo wa Ubelgiji wa miaka 28, amefanikiwa kufunga mabao matano pekee ya Ligi ya Primia katika mechi 17 tangu ajiunge tena na mabingwa watetezi wa Ligi ya Mabingwa Chelsea msimu huu, na kufunga mabao mengine matano katika mashindano mengine.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved