logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mzozo wa Ukraine: Poland yasusia mechi ya kufuzu kwa fainali ya Kombe la Dunia dhidi ya Urusi

Hii ni kutokana na uvamizi wa Urusi dhidi ya Ukraine

image
na Radio Jambo

Yanayojiri26 February 2022 - 14:02

Muhtasari


•Poland haitacheza mechi ya mchujo ya Kombe la Dunia la 2022 dhidi ya Urusi mjini Moscow mnamo Machi 24 kutokana na uvamizi wa Urusi dhidi ya Ukraine

Poland haitacheza mechi ya mchujo ya Kombe la Dunia la 2022 dhidi ya Urusi mjini Moscow mnamo Machi 24 kutokana na uvamizi wa Urusi dhidi ya Ukraine, rais wa shirikisho la soka la Poland amesema.

"Hakuna maneno zaidi, ni wakati wa kuchukua hatua," Cezary Kulesz alisema. Alisema Poland ilikuwa inazungumza na mashirikisho ya soka ya Czech na Uswidi ili kuwasilisha msimamo mmoja kwa shirikisho la soka duniani FIFA.

Urusi inatazamiwa kuwa mwenyeji wa Poland mjini Moscow tarehe 24 Machi, huku Ukraine ikisafiri hadi Scotland siku hiyo hiyo.

Wakati huo huo kiungo wa kimataifa wa Poland Robert Lewandowski ameunga mkono hatua ya nchi yake kususia mechi ya kufuzu kwa fainali ya Kombe la Dunia dhidi ya Urusi baada ya uvamizi wa Ukraine, akisema "hatuwezi kujifanya kuwa hakuna kinachoendelea".

Mshambulizi huyo wa Bayern Munich Lewandowski, 33, ambaye ni mfungaji bora wa mabao nchini mwake, aliongeza: "Siwezi kucheza mechi na timu ya taifa ya Urusi wakati nchi hiyo ikiendelea na uvamizi wake dhidi ya Ukraine.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved