logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Thiery Henry afunguka kuhusu msongo wa mawazo baada ya kugura Arsenal

Alifichua ilimchukua zaidi ya mwaka mmoja kutulia Barcelona kutokana na yale ambayo alikuwa anapitia.

image
na Radio Jambo

Burudani10 March 2022 - 07:39

Muhtasari


•Wakati huo, Mfaransa huo alikuwa anapambana na jeraha la muda mrefu na alikuwa kwenye harakati ya kutengana na aliyekuwa mkewe Claire Merry.

•Henry alifichua ilimchukua zaidi ya mwaka mmoja kutulia Barcelona kutokana na yale ambayo alikuwa anapitia.

Mshambulizi wa zamani wa Arsenal na Ufaransa

Mwanasoka wa zamani Thierry Henry amefunguka kuhusu alivyoathirika kisaikolojia baada ya kugura klabu ya Arsenal takriban miaka 15 iliyopita.

Mnamo mwaka wa 2007 Henry alijiunga na Barcelona baada ya kuchezea The Gunners kwa zaidi ya mwongo mmoja.

Wakati huo, Mfaransa huo alikuwa anapambana na jeraha la muda mrefu na alikuwa kwenye harakati ya kutengana na aliyekuwa mkewe Claire Merry.

Henry alilazimika kulipa mkewe zaidi ya pauni milioni kufuatia talaka yao iliyokuja takriban miaka mitano tu baada ya kufunga ndoa. Wawili hao walikuwa na binti mmoja pamoja.

Akiwa kwenye mahojiano na L'Equipe, Henry alifichua ilimchukua zaidi ya mwaka mmoja kutulia Barcelona kutokana na yale ambayo alikuwa anapitia.

"Nilipoondoka Arsenal kwenda Barcelona ilinichukua mwaka mmoja kuwa sawa.  Nilifika nikiwa na jeraha na nilikuwa katika harakati ya talaka, lazima ningejifunza mfumo mpya, yote hayo yalifanya nichangikiwe akili," Alisema.

Gwiji huyo wa timu ya taifa ya Ufaransa alisema wakati huo ilikuwa ngumu kufunguka kuhusu hali ya kisaikolojia.

Henry hakuwa kutoa mchango mkubwa sana pale Barcelona kama ilivyokuwa akiwa Arsenal. Hata hivyo aliweza kunyakua vikombe viwili vya Laliga na Champions League moja akiwa na mabingwa hao wa Uhispania.

Aliondoka Barca mwaka wa 2010 na kujiunga na New York Red Bulls ya Marekani.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved