logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Hongera!Nahodha wa Manchester United Harry Maguire amefunga pingu za maisha

Waliandamana na familia na marafiki.

image
na Radio Jambo

Burudani26 June 2022 - 08:07

Muhtasari


  • Nahodha wa Manchester United Harry Maguire amefunga pingu za maisha

Nahodha wa Manchester United Harry Maguire amefunga pingu za maisha na mpenzi wake wa muda mrefu Fern Hawkins.

Wawili hao ambao wamekuwa pamoja kwa miaka 11, walifunga ndoa katika ukumbi wa Chateau de Varennes nchini Ufaransa siku ya Jumamosi.

Waliandamana na familia na marafiki.

Katika ujumbe wa kufurahisha moyo kwenye Instagram, nyota huyo  alishiriki picha ya kupendeza akimbusu mkewe, akiwa amevalia suti ya kijivu iliyomkaa huku Hawkins aking'aa katika gauni jeupe linalong'aa.

Aliandika, "Siku ambayo sitaisahau."

Wenzi hao walitangaza kuchumbiana kwao mnamo 2018 wakati wa safari ya kimapenzi kwenda Paris.

Mshabiki na marafiki walimpongeza mchezaji huyo kwa hatua yake mpya maishani.

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved