logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Aliyekuwa kocha wa Wolves na Spurs apata kazi ya ukocha Saudia

Kando na Tottenham Hotspurs na Wolves, Nuno Espirito Santo pia aliwahi funza vilabu vya Valencia na Porto.

image
na Radio Jambo

Yanayojiri06 July 2022 - 05:55

Muhtasari


• Nuno akiwa kocha mkuu wa Wolves alisaidia timu hiyo kumaliza nambari saba kwenye jedwali kwa mara zaidi ya moja.

Kocha Nuno Espirito Santo na mmiliki wa klabu ya Al Ittihad

Baada ya kukaa nje kwenye kijibaridi kwa zaidi ya mwaka mmoja, hatimaye aliyekuwa kocha mkuu wa Tottenham Hotspurs kutokea Uingereza, Mreno Nuno Espirito Santo amepata kibarua chenye mshahara mnono.

Kocha huyo ambaye kwa wakati mmoja aliwahi kuifunza timu ya Wolves kabla ya kuigura na kuingia Spurs alijipata pabaya kikazi baada ya timu ya Spurs kuvurunda katika matokeo na kujipata pabaya katika msimamo wa ligi kuu nchini Uingereza.

Nuno Espirito Santo amefanikiwa kupata kazi katika timu moja kutokea Saudia kwa jina Al Ittihad kama kocha mkuu.

Santo aliingia kwenye mkataba na miamba hao wa taifa hilo la jangwani na atakuwa anawanoa makali hadi mwaka 2024.

Santo ana uzoefu mkubwa kama kocha kwani kabla ya kutimba Uingerezea kuvitumikia vilabu vya Wolves na Tottenhma, aliwahi noa makali ya vilabu vya Valencia kutoka Uhispania na Porto ya nyumbani kwao Ureno.

Mkufunzo huyo jina lake halitawahi futika katika kumbukumbu za mashabiki ugani Molineux ambapo aliisaida Wolves kuwa tishio kwa baadhi ya timu kubwa kwenye ligi kuu ya EPL, kando na kusaidia timu hiyo kumaliza ligi katika nafasi ya saba kwenye jedwali kwa zaidi ya mara moja.

Kila la kheri Nuno katika kibarua chako kipya!


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved