logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Rasmi! Makubaliano yaafikiwa kuhusu uhamisho wa Casemiro kujiunga na Mashetani Wekundu

Casemiro ameigharimu Manchester United Euro milioni 60 na nyongeza na Euro milioni 10.

image
na Radio Jambo

Habari20 August 2022 - 06:27

Muhtasari


•Manchester United imefikia makubaliano na Real Madrid kuhusu uhamisho wa kiungo matata Carlos Henrique Casemiro.

•Real Madrid tayari imemuaga kiungo huyo na kusherehekea ushindi alioupata tangu ajiunge nao Januari 2013.

Klabu ya Manchester United imefikia makubaliano na Real Madrid kuhusu uhamisho wa kiungo matata Carlos Henrique Casemiro.

Katika taarifa iliyotolewa Ijumaa jioni, United ilitangaza kuwa mchezaji huyo wa timu ya kitaifa ya Brazil mwenye umri wa miaka 30 atajiunga nao rasmi baada ya makubaliano ya masharti ya kibinafsi.

"Tunatazamia kumkaribisha Casemiro Old Trafford," Taarifa iliyochapishwa kwenye tovuti rasmi ya United ilisoma.

Casemiro anaripotiwa kuwagharimu Mashetani Wekundu Euro milioni 60 na nyongeza na Euro milioni 10.

Amekubali kutia saini mkataba wa miaka minne hadi 2027  na anatazamiwa kusafiri hadi Mancheter wikendi hii kwa ajili ya vipimo vya kidaktari.

Real Madrid tayari imemuaga kiungo huyo na kusherehekea ushindi alioupata tangu ajiunge nao Januari 2013.

"Real Madrid ingependa kutoa shukrani za dhati kwa Casemiro, ambaye ni sehemu ya historia ya klabu hii," Mabigwa hao wa Uhispania walisema katika taarifa.

Klabu hiyo pia ilitangaza kuwa hafla ya kumuaga rasmi Casemiro itafanyika Jumatatu kisha ahutubie waandishi wa habari.

"Real Madrid ndio nyumbani kwake na daima, na tunamtakia kila la heri yeye na familia yake katika sura hii mpya ya maisha yake."

Usajili huu umejiri huku Mashetani Wekundu wakitazamiwa kucheza na Liverpool Jumatatu. Klabu hiyo itatumai kuwa kiungo huyowa kati  mwenye kipawa ataweza kushiriki katika mechi hiyo kali itakayochezewa Old Trafford.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved