logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Kwa miaka yote nilicheza Uingereza, nilihisi upendo wa Malkia - Ronaldo

"Kwa miaka hii yote, nimehisi upendo wa milele wa Uingereza kwa Malkia, na jinsi Ukuu wake ulivyokuwa muhimu" - Ronaldo

image
na Radio Jambo

Habari10 September 2022 - 07:23

Muhtasari


• “Ninalipa heshima yangu kwa kumbukumbu yake na ninaomboleza msiba huu usioweza kubadilishwa" - Ronaldo

Ronaldo amemuomboleza malkia Elizabeth

Mwanasoka maarufu zaidi duniani kwenye mtandao wa Instagram, Mreno Christiano Ronaldo amekuwa mtu wa hivi punde kumuomboleza malkia wa Uingereza, Elizabeth wa paliteaga dunia usiku wa Alhamis.

Kupitia mitandao yake ya kijamii, Christiano alimtaja malkia Elizabeth wa pili kama mtu ambaye hatoweza kusahaulika katika historia ya soka na haswa katika maisha akianza kukipiga kwenye ligi kuu ya Uingereza EPL miaka ya mapema 2000.

Ronaldo alikumbuka alipojiunga kwenye Klabu ya Manchester United akiwa kinda jinsi alivyohisi mazingira ya Uingereza yote yalikuwa yamehanikiza upendo wa watu wake kwa maalkia wao na jambo hilo lilimfanya pia kupenda jinsi malkia alivyokuwaanaenziwa kutokana na uongozi wake weney mfano wa kudumu.

“Miaka saba ya maisha yangu ya uchezaji ilichezwa katika Ligi ya Premia, na kufanya huu kuwa msimu wangu wa 8 kuishi Uingereza. Kwa miaka hii yote, nimehisi upendo wa milele wa Uingereza kwa Malkia, na jinsi Ukuu wake ulivyokuwa muhimu na utakuwa milele kwa watu wa Uingereza,” Ronaldo aliandika.

Mchezaji huo ambaye ni binadamu mwenye ufuatiliaji mkubwa wa umati kwenye mtandao wa Instagram alimuomboleza na kutoa rambirambi zake kwa kusema kwamba kumpoteza malkia Elizabeth wa pili ni pengo ambalo halitakuja kuzibika kabisa kwa miaka na mikaka.

“Ninalipa heshima yangu kwa kumbukumbu yake na ninaomboleza msiba huu usioweza kubadilishwa na nchi ambayo nimejifunza kuiita nyumbani. Mawazo yangu na maombi ni pamoja na Familia ya Kifalme,” Mreno Ronaldo aliandika.

Kufuatia kifo cha malkia huyo mwenye umri wa miaka 96, jana bodi inayosimamia ligi ya premia nchini Uingereza ilikutana na kwa pamoja kuafikiana kuahirisha ligi hiyo mpaka pale malkia atakapozikwa kama njia moja ya kumuenzi na kutoa heshima za mwisho kwa msiba wake.

Awali, Uingereza ilitangaza siku kumi na mbili za maombolezi katika taifa hilo huku shughuli zote muhimu za kuwakusanya watu pamoja ikiwemo michezo, Sanaa na siasa zikisitishwa katika kipindi hicho cha siku kumi na mbili za maombolezi.

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved