logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Kombe la Dunia Qatar 2022: Ukweli kuhusu Sadio Mané

Tangu akiwa na umri mdogo alitamani kuwa mchezaji soka.

image
na Radio Jambo

Habari11 November 2022 - 08:29

Sadio Mane mwenye umri wa miaka 30, ni mmoja wa wachezaji bora zaidi wa soka duniani kwa sasa. Huku akijiandaa kuiwakilisha nchi yake Senegal katika Kombe la Dunia la Qatar 2022, huu ndio ukweli kumhusu.

  • Mané mwenye alizaliwa katika kijiji cha Bambali, Sédhiou, nchini Senegal
  • Tangu akiwa na umri mdogo alitamani kuwa mchezaji soka
  • Baba yake yake ambaye alikuwa Iman alimzuia kucheza soka alipokuwa mtoto
  • Lakini akiwa na umri wa miaka saba, baba yake alifariki na alipotimiza umri wa miaka 15, alitoroka kijijini kwao kwenda katika mji mkuu Dakar kutekeleza azma yake ya kuwa mwanasoka.
  • Mwaka 2009, wakati alipokuwa akichezea timu ya M’Bour ligunduliwa na maskauti na baadaye alitambuliwa na Génération Foot,
  • Mwaka 2011 alijiunga na klabu ya Metz, ambayo ilikuwa na ushirika na Génération Foot
  • Alijiunga na klabu ya Austria ya Salzburg tarehe 31 Agosti 2012
  • Baadaye alijiunga na klabu ya Southampton na kuichezea katika msimu wa mwaka 2014- 2015
  • Mwaka 2016 hadi 2022 aliichezea klabu ya Liverpool lakini tarehe 22 June, 2022 alijiunga na klabu ya Ligi ya ujerumani Bundesliga, Buyern Munich.

RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved