logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Arsenal wakiendelea hivi hatutawafikia, huenda wakapita pointi 100 - Pep Guardiola

Alisema kuwa timu hiyo ya Arteta ina wastani wa kufikisha alama nyingi msimu huu.

image
na Radio Jambo

Habari05 January 2023 - 12:05

Muhtasari


• Licha ya kukiri kuwa Arsenal ni timu nzuri, Guardiola alisema watajitahidi ili kuwang'atua kileleni mwa jedwali, huku akitumai watapoteza pointi.

Guardiola aipigia upato Arsenal kufika pointi 100

Mkufunzi wa Manchester City Pep Guardiola amefunguka wasiwasi wake kuhusu ligi ya Premia ya Uingereza huku timu yake wakijiandaa Alhamisi hii usiku kumenyana na Chelsea wakijaribu kubana mwanya kati yao na viongozi Arsenal.

Katika mahojiano na wanahabari mbele ya mechi hiyo ya Stamford Bridge, Guardiola aliuliziwa kuhusu Arsenal na uwezekano wao kushinda ubingwa wa ligi ya Premia msimu huu.

Guardiola alikiri kuwa vijana wa Arteta wako imara msimu huu kinyume na misimu ya nyuma na kusema wakiendelea na uzuri wao ambao wako nao kwa sasa, basi itakuwa vigumu kwa timu yoyote, ikiwemo Man City kuing’atua Arsenal kileleni mwa jedwali.

Alisema kuwa wakiendelea hivyo huenda watafikisha pointi zaidi ya 100 kwenda mbele na kuandikisha rekodi mpya, akisema kuwa ushindi wao katika mechi zilizopita unaonesha kuwa wako katka uwastani wa kufikisha pointi hizo.

“Arsenal wana wastani wa kufikisha pointi 100 - au zaidi ya pointi 100. Wakiendelea hivyo, hatutawapata,” Guardiola mwenye wasiwasi wa kutetea ubingwa huo kwa mara ya tatu mtawalia alisema.

Licha ya kuwapa Arsenal asilimia kubwa ya kushinda ligi hiyo, Guardiola alisisitiza kuwa vita bado vingalipo na mapambani yataendelea mpaka tone la mwisho la jasho huku akisema kuwa timu yake wanajitahidi kuwa karibu na uzuri kama wa Arsenal ili kuwapa kibarua kigumu kileleni.

“Kwa hivyo inabidi tuwe wakamilifu kuanzia hapa hadi mwisho wa msimu na kutumaini kwamba watashuka kidogo katika viwango vyao,” alisema.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved