logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Tulikusanya zaidi ya Ksh 3M kutoka kwa debi ya Mashemeji - AFC Leopards

Mechi baina ya Leopards na Gor Mahia iliishia sare kapa katika uwanja wa Nyayo.

image
na Radio Jambo

Habari31 January 2023 - 10:49

Muhtasari


• Leopards walikuwa wenyeji wa mechi hiyo na walisema ndio ilikuwa mechi ya kwanza ya msimu kuuza tikiti nyingi.

Mashabiki wa AFC Leopards wakisherehekea baada ya mechi

Klabu ya AFC Leopards ambao ndio walikuwa wenyeji katika mechi ya Mashemeji iliyofanyika wikendi iliyopita ugani Nyayo Nairobi imetangaza kutengeneza pesa nyingi kutokana na mechi hiyo.

Kupitia taarifa ambayo Leopards walichapisha mitandaoni, walisema kuwa mechi hiyo iliandikisha historia kama moja ambayo ilipata mafanikio makubwa, mashabiki wengi wakijitokeza kuhudhuria katika miaka ya hivi karibuni.

Leopards ilisema ilitengeneza shilingi milioni 3.3 kutoka kwa viingilio ambapo tikiti za kawaida za shilingi 300 zilinunuliwa na mashabiki 9,565 huku zile za sehemu maalum almaarufu VIP ambazo zilikuwa zinauzwa kwa shilingi elfu moja zikinunuliwa na watu 461.

Leopards waliwashukuru mashabiki na washikadau wa soka nchini kwa kujitokeza kwa wingi na kuhudhuria mechi hiyo, huku wakisema ni ishara nzuri ya kuonesha mafanikio makubwa katika soka la Kenya ambalo limefifia katika miaka michache iliyopita.

“Zaidi ya tikiti 10,000 ziliuzwa kwa wikendi ya #MashemejiDerby, na kuifanya kuwa mechi yetu iliyohudhuriwa na watu wengi zaidi kwenye ligi msimu huu hadi sasa. Tiketi 461 kati ya hizo zilikuwa za sehemu ya VIP na 9565 zilikuwa za matuta. Kwa mara nyingine tena asante kwa kujitokeza na kufanya mechi kuwa hai,” AFC Leopards walitoa taarifa.

Mechi hiyo iliisha kwa sare kappa huku Leopards wakisalia katika nafasi ya 8 kwa alama 18 na Gor Mahia wakipanda hadi nafasi ya pili kwa alama 24 nyuma ya viongozi Nzoia Sugar wenye alama 27.

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved