logo

NOW ON AIR

Listen in Live

CR7 ashinda tuzo yake ya kwanza katika ligi ya Saudia, miezi 2 tu tangu kwenda Al Nassr

Ronaldo alituzwa kama mchezaji bora wa mwezi Februari.

image
na Radio Jambo

Habari05 March 2023 - 08:22

Muhtasari


• Tangu ajiunge na klabu yake mpya, Ronaldo amefunga mabao manane na kutoa pasi mbili za mabao.

• Ronaldo alifunga bao lake la kwanza la Al Nassr katika sare yao ya 2-2 dhidi ya Al Fateh mnamo Februari 3

Ronaldo akiwa na tuzo ya Roshn kama mchezaji bora wa Februari.

Staa wa soka kutoka Ureno Christiano Ronaldo ameshinda tuzo yake ya kwanza kama mchezaji wa Al Nassr katika ligi kuu nchini Saudi Arabia, miezi miwili tu baada ya kuhamia katika taifa hilo la Uarabuni.

Ronaldo alituzwa kama mchezaji bora wa mwezi Februari maarufu kwa jina Roshn na alionesha furaha yake akisema kwamba ndio mwanzo anafungua rafu ya tuzo zake katika ligi hiyo mpya kwake.

“Nina furaha kushinda tuzo ya Mchezaji Bora wa mwezi wa Februari kwa Ligi ya Roshn Saudi. Natumai ya kwanza kati ya nyingi! Najivunia kuwa sehemu ya timu hii Al-Nassr,” Ronaldo alisema kweney mitandao ya kijamii.

CR7 aliwasili Al Nassr baada ya klabu hiyo ya Saudia kufanikiwa kumsajili kwa mkataba wa hali ya juu mwezi Januari. Mchezaji huyo wa kimataifa wa Ureno amepata mdundo wake haraka katika Ligi ya Saudi Pro, akicheza jukumu muhimu katika safu ya ushambuliaji ya timu yake.

Tangu ajiunge na klabu yake mpya, Ronaldo amefunga mabao manane na kutoa pasi mbili za mabao. Maonyesho ya CR7 yamesaidia Al Nassr kudumisha nafasi yao kileleni mwa jedwali la Saudi Pro League.

Ronaldo alifunga bao lake la kwanza la Al Nassr katika sare yao ya 2-2 dhidi ya Al Fateh mnamo Februari 3. Kisha akafunga mabao yote manne ya timu yake dhidi ya Al Wehda wiki moja baadaye.

CR7 alikamilisha maonyesho yake mazuri mwezi Februari kwa kufunga hat-trick katika ushindi wa 3-0 wa Al Nassr dhidi ya Damac wiki iliyopita. Ushindi huo uliwaweka Ronaldo na wenzake kileleni mwa jedwali la Saudi Pro League, pointi mbili juu ya Al Ittihad.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved