logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mashetani Wekundu wabanduliwa nje Europa

United walikuwa chini ya kiwango chao na walizidiwa nguvu karibu kila dakika.

image
na Radio Jambo

Habari21 April 2023 - 04:44

Muhtasari


•United walifanya makosa mawili mabaya katika safu yao ya ulinzi -yaliyowagharimu kwa kuchapwa 3-0.

•Katika mechi ya kwanza Old Trafford wakiwa mbele kwa mbwembwe kwa mabao 2-0, yakarudi na kwenda sare ya 2-2.

Manchester United imefungasha virago michuano ya Ulaya baada ya kuchapwa na Sevilla katika mzunguko wa pili wa robo fainali ya Ligi ya Europa.

United walikuwa chini ya kiwango chao – walizidiwa karibu kila idara na mbaya zaidi walifanya makosa mawili mabaya katika safu yao ya ulinzi -yaliyowagharimu kwa kuchapwa 3-0.

Katika mechi ya kwanza Old Trafford wakiwa mbele kwa mbwembwe kwa mabao 2-0, yakarudi na kwenda sare ya 2-2.

Kikosi hicho cha Erik ten Hag ni kama kimeruhusu mabao matano ndani ya dakika 90 - mabao mawili ya dakika za mwisho huko Manchester na matatu Jana Hispania.

Sevilla iko nafasi ya 13 kwenye Ligi Hispania (La Liga) na wametumia muda mwingi wa msimu mbaya kupambana kukwepa kushuka daraja, lakini walionekana kuimarika tena chini ya Jose Luis Mendilliba, meneja wao wa tatu wa kudumu msimu huu.

Sevilla sasa itakutana na Juventus iliyoiondosha Sporting CP kwa jumla ya mabao 2-1, kufuatia sare ya 1-1 jana. Mchezo wa awali Juve ilishinda 1-0.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved