logo

NOW ON AIR

Listen in Live

‘Taji lipo mikononi mwetu’ Guardiola asema baada ya Manchester City kuizaba Arsenal mabao 4-1

• Kikosi cha Pep Guardiola, sasa kiko pointi mbili nyuma ya Arsenal kikiwa na michezo miwili mkononi.

image
na Radio Jambo

Habari27 April 2023 - 04:30

Muhtasari


• Kikosi cha Pep Guardiola, sasa kiko pointi mbili nyuma ya Arsenal kikiwa na michezo miwili mkononi.

Pep Guardiola anasema kuwa kikosi chake cha Manchester City kimethibitisha kuwa kinaweza kufanya kazi wakati hakuna "chaguo zaidi ila kushinda" baada ya kuishinda Arsenal na kuweka mikononi mwao kinyang’anyiro cha kushinda ubingwa wa Ligi ya Premia .

Kikosi cha Guardiola kiliwashinda viongozi Arsenal 4-1 kwenye Uwanja wa Etihad, na sasa wako nyuma kwa pointi mbili wakiwa na michezo miwili ya ziada .

City wamebakisha mechi saba, wakianza na safari ya Jumapili dhidi ya Fulham kabla ya mechi za nyumbani dhidi ya West Ham na Leeds.

"Hatuwezi kupoteza umakini wetu. Sasa iko mikononi mwetu," alisema Guardiola.

Manchester City walifanya vyema na kuwalemea viongozi wa Ligi ya Premia Arsenal na kuwapa pigo kubwa la kisaikolojia katika jitihada za kushinda ubingwa wa ligi huko Etihad .

Makabiliano hayo yaliyodaiwa kuwa mwamuzi wa taji yaligeuka na kuwa jambo la aibu kwa upande mmoja.

Kikosi cha Pep Guardiola, sasa kiko pointi mbili nyuma ya Arsenal kikiwa na michezo miwili mkononi, kilichochewa na ushirikiano hatari wa Erling Haaland na Kevin de Bruyne.

City wanaweza kwenda kileleni kwa ushindi dhidi ya Fulham siku ya Jumapili huku Arsenal wakilazimika kwa namna fulani kujiondoa kwenye mdororo ambao umewafanya kucheza mechi nne za ligi bila kushinda katika hatua muhimu ya msimu huu.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved