logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Nani anafaa kuwa nahodha mpya wa Man Utd baada ya Maguire kupokonywa wadhifa huo?

Vyanzo vya karibu na Maguire vimesisitiza kwa miezi kadhaa kuwa anataka kusalia United.

image

Michezo17 July 2023 - 15:32

Muhtasari


  • Wakati Manchester United ilipolipa rekodi ya £80m kumfanya Harry Maguire kuwa beki ghali zaidi duniani mwaka 2019, moja ya vivutio vikubwa ni uwezo wake wa kuongoza.

Beki wa Uingereza Harry Maguire ameambiwa hatakuwa nahodha wa Manchester United msimu ujao - je huo ndio uamuzi sahihi? Na hilo linaacha wapi mustakabali wa Maguire Old Trafford?

Bruno Fernandes aliongoza kikosi hicho mara nyingi msimu uliopita - je, yeye ndiye mchezaji sahihi kuchukua adhfa huo? Au kuna mgombea mwingine ambaye Erik ten Hag anafaa kumchagua?

Wakati Manchester United ilipolipa rekodi ya £80m kumfanya Harry Maguire kuwa beki ghali zaidi duniani mwaka 2019, moja ya vivutio vikubwa ni uwezo wake wa kuongoza.

Ndani ya miezi mitatu baada ya kuwasili kutoka Leicester, Maguire alikuwa nahodha wa klabu hiyo ya Old Trafford kwa mara ya kwanza. Chini ya miezi mitatu baada ya hapo, Muingereza huyo alipewa kitambaa hicho kwa misingi ya kudumu baada ya Ashley Young kuhamia Inter Milan.

Sasa Maguire amevuliwa unahodha na bila shaka ndiye beki wa kati chaguo la tano wa Erik ten Hag katika United.

Huku Euro 2024 ikikaribia mwisho wa msimu huu ujao, kocha wa Uingereza Gareth Southgate amemwambia Maguire anahitaji kucheza mara nyingi zaidi ili kupata nafasi yake kwenye kikosi.

Vyanzo vya karibu na Maguire vimesisitiza kwa miezi kadhaa kuwa anataka kusalia United. Lakini kwa mwisho gani?

Vilabu vingine, ikiwemo West Ham, vinamtaka Maguire. Swali linapaswa kuulizwa, je, huu ni wakati wa kuondoka?

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved