logo

NOW ON AIR

Listen in Live

“Nitakuwa PSG hata bila ya mapenzi yenu” Neymar kwa mashabiki waliomtaka kuondoka

PSG walizama mfukoni mwaka 2017 ambapo walitoa kima cha Euro 222 kwa Barcelona.

image
na Davis Ojiambo

Michezo20 July 2023 - 09:00

Muhtasari


  • • Neymar mpaka sasa ndiye anayeshikilia rekodi ya uhamisho wa hela ndefu Zaidi katika soka la kisasa.
  • • PSG walizama mfukoni mwaka 2017 ambapo walitoa kima cha Euro 222 kwa Barcelona, rekodi ambayo haijapata kuvunjwa hadi sasa.
Neymar Junior

Mchezaji wa kimataifa wa Brazili na klabu ya PSG ya Ufaransa Neymar Jr ameweka wazi kuhusu mustakabali wake katika klabu hiyo.

Neymar ambaye alikosa sehemu kubwa ya msimu uliokamilika kutokana na msururu wa majeraha amesema kwamba yeye anaona mustakabali wake ukiwa bado katika klabu hiyo licha ya kwamba mashabiki hawamtaki.

Akizungumza na Caze TV, Neymar alisema kwamba anatumai msimu kesho atashiriki katika kampeni ya PSG kwa kile alisema kwamba bado ana mkataba nao na hajaambiwa chochote kuhusu kutemwa kwake au kuuzwa kwenda kwa timu nyingine.

Neymar pia aliwapa ujumbe mashabiki walioingia nyumbani kwake mwishoni mwa msimu kwa fujo wakimpa ujumbe wa kuondoka katika timu yao, akisema kuwa hata bila ya mapenzi yao kwake, bado tu ataisakatia PSG.

“Natumai mustakabali wangu bado utakuwa PSG msimu kesho. Niko na mkataba na hakuna mtu yeyote ameniambia kitu chochote kuhusu kuondoka. Hata kama hakuna mapenzi makubwa baina yangu na mashabiki, bado nitakuwepo PSG, na mapenzi yao au bila mapenzi yao,” Neymar alisema.

Mchezaji huyo amekuwa akihusishwa na uhamisho kwenda vilabu vingi tu vya ligi kuu ya Uingereza ikiwemo Chelsea na Manchester United.

Neymar mpaka sasa ndiye anayeshikilia rekodi ya uhamisho wa hela ndefu Zaidi katika soka la kisasa.

PSG walizama mfukoni mwaka 2017 ambapo walitoa kima cha Euro 222 kwa Barcelona, rekodi ambayo haijapata kuvunjwa hadi sasa.

Msimu ambao umekamilika ulikuwa mbaya kwake haswa katika kipindi cha pili, pindi baada ya kuondoka katika mashindano ya kombe la dunia ambapo Brazili walitemwa kwa matuta ya penalty ya Croatia katika awamu ya robo fainali.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved