logo

NOW ON AIR

Listen in Live

AFL: Rais wa FIFA Gianni Infantino awasisimua mashabiki kwa ujuzi wake wa Kiswahili

“Simba nguvu moja!! Simba nguvu moja!!” Infantino alisema kwa Kiswahili

image
na Radio Jambo

Habari21 October 2023 - 09:15

Muhtasari


•Ilikuwa ni wakati akiitambulisha Simba SC ya Tanzania ambapo alizungumza lugha ya Kiswahili na kuwasisimua maelfu ya mashabiki.

•Bosi huyo wa FIFA aliitaja Ligi hiyo mpya ya Soka ya Afrika kuwa mashindano bora zaidi ya kandanda barani Afrika 

Gianni Infantino aliwasisimua mashabiki wa soka kwa ujuzi wake wa Kiswahili Ijumaa.

Rais wa FIFA Gianni Infantino aliwasisimua mashabiki wa soka kwa Kiswahili chake siku ya Ijumaa wakati akitoa hotuba yake kwenye sherehe za ufunguzi wa Ligi ya Soka ya Afrika (AFL) kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam, Tanzania.

Infantino alikuwa miongoni mwa wageni mashuhuri wa kimataifa waliopamba hafla ya ufunguzi wa ligi hiyo mpya ya Afrika ambayo inatazamiwa kubadilisha soka la klabu barani.

Rais alipongeza Shirikisho la Soka barani Afrika (CAF) kwa juhudi zake za kuandaa ligi ya kandanda akiitaja kuwa ushahidi wa dira na kujitolea kwao katika mchezo huo unaopendwa na mabilioni ya mashabiki kote duniani.

"Nataka kumshukuru Rais wa CAF, Patrice Motsepe, na soka zima la Afrika kwa juhudi zao za kuendeleza soka barani Afrika," alisema Bw Infantino kwa Kiingereza.

Rais huyo wa FIFA pia alitambua vilabu viwili vilivyokuwa vifungue shindano hilo, Simba SC ya Tanzania na Al Alhy ya Algeria.

Ilikuwa ni wakati akiitambulisha Simba SC ya Tanzania ambapo alizungumza lugha ya Kiswahili na kuwasisimua maelfu ya mashabiki waliokuwa wamekusanyika uwanjani.

“Simba nguvu moja!! Simba nguvu moja!!” Infantino alisema kwa Kiswahili mashabiki wakishangilia na kuinua mabango ya Simba.

Aliendelea, “Karibu Tanzania.. huu ni upendo, huu ni upendo, hii ni Tanzania, hii ni Afrika, hii ni Simba, hii ni Al Ahly, hii ni CAF, hii ni FIFA na hii ni mpira. Soka inaunganisha dunia na leo soka inaunganisha dunia kutoka Tanzania.”

Bosi huyo wa FIFA aliitaja Ligi hiyo mpya ya Soka ya Afrika kuwa mashindano bora zaidi ya kandanda barani Afrika na fursa nzuri kwa vilabu vya Kiafrika kuwa katika medani ya kandanda ya kimataifa.  Aliwaomba Waafrika kufurahia shindano hilo kwani linaanza safari inayotarajiwa kuwa ya kuvutia.

Alimalizia hotuba yake kwa kusema , “Asante sana!” kwa lugha ya Kiswahili.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved