Graham Potter kuchukua mikoba ya ukufunzi Man Utd endapo Erik Ten Hag atafukuzwa kazi

Lakini ikiwa Reds Devils wanataka kumwajiri Potter, itabidi wachukue hatua haraka kwani Muingereza huyo pia anasakwa na Napoli.

Muhtasari

• Kocha wa zamani wa Chelsea, Tottenham na Inter Milan Antonio Conte pia anazingatiwa.

• Hata hivyo, gazeti la The Sun linaripoti kwamba Potter anavutiwa sana na Sir Jim Ratcliffe na atakuwa mgombea anayeongoza kuchukua nafasi ya Ten Hag

Graham Potter na Erik Ten Hag
Graham Potter na Erik Ten Hag
Image: X

Meneja wa zamani wa Chelsea Graham Potter ndiye anayewania nafasi kubwa ya kuinoa Manchester United iwapo Erik ten Hag ataondoka, kulingana na ripoti ya Metrok UK.

Lakini ikiwa Reds Devils wanataka kumwajiri Potter, itabidi wachukue hatua haraka kwani Muingereza huyo pia anasakwa na Napoli.

Mkufunzi huyo mwenye umri wa miaka 48 amekuwa nje ya kazi tangu alipotimuliwa na Chelsea mwezi Aprili baada ya kukaa kwa miezi saba Stamford Bridge.

Alishinda michezo 12 pekee kati ya 31 akiwa kocha wa The Blues, licha ya uwekezaji mkubwa kwenye kikosi hicho, huku klabu hiyo ikimaliza nafasi ya 12 kwenye Ligi Kuu.

Walakini, Potter bado ana sifa nzuri kutokana na kazi yake nzuri huko Brighton na tangu wakati huo amekuwa akihusishwa na vilabu mbali mbali, vikiwemo Nice, Leicester, Crystal Palace, Rangers na Lyon.

Lakini inasemekana Potter anasubiri nafasi katika klabu ya Ligi ya Mabingwa, habari ambazo zitawafurahisha Napoli ambao wanavutiwa na huduma yake huku mabingwa hao wa Serie A wakihangaika chini ya Rudi Garcia ambaye alichukua tu msimu wa joto.

Kocha wa zamani wa Chelsea, Tottenham na Inter Milan Antonio Conte pia anazingatiwa.

Hata hivyo, gazeti la The Sun linaripoti kwamba Potter anavutiwa sana na Sir Jim Ratcliffe na atakuwa mgombea anayeongoza kuchukua nafasi ya Ten Hag wakati mmiliki wa Ineos atakapokamilisha unyakuzi wake kwa sehemu Old Trafford.

Ratcliffe anatazamiwa kununua asilimia 25 ya hisa za klabu hiyo kwa takriban pauni bilioni 1.5 na kudhibiti uendeshaji wa soka.

Kama ilivyotajwa, mmiliki wa Nice alijaribu kumvuta Potter kwa upande wa Ufaransa mapema mwaka huu, na anaweza kujaribu tena ikiwa Ten Hag ataondolewa majukumu yake.