Olunga amshukuru Mungu kwa kufunga bao na asisti dhidi ya timu ya Ronaldo na Mane

"Asante Bwana kwa bao na asisti. Utukufu wote ni wako. Mwanzo wa mambo makubwa zaidi yanayokuja,” Olunga alishukuru Mungu.

Muhtasari

• Katika mpambano huo mkali, Cristiano Ronaldo alifunga mabao mawili ya hali ya juu huku Al Nassr wakiendeleza rekodi yao nzuri.

Olunga na Ronaldo
Olunga na Ronaldo
Image: Facebook

Nahodha wa timu ya taifa Harambee Stars, Michael Olunga anayecheza katika ligi ya Qatar kwa timu ya Al Duhail amemshukuru Mungu kwa kuifunga Al Nassr yake Ronaldo na Mane kutoka Saudi Arabia bao na pia kutoa asisti.

Mechi hiyo ilichezewa nchini Saudi Arabia usiku wa Jumanne katika mashindano ya kombe la klabu bingwa barani Asia.

Licha ya Al Duhail yake Olunga kupoteza kwa mabao 4-3 mikononi mwa kikosi mahiri cha Al Nassr, Olunga alifanikiwa kufunga bao moja na kutoa asisti katika ushinde wao.

Kwake ni mchezo wa kujivunia kushiriki uwanja mmoja na mastaa kama Ronaldo lakini akaahidi kwamba watajitahidi na kujitutumua kisabuni kurejesha ushindi katika mechi ya marudiano nchini Qatar.

“Onyesho kubwa katika mpambano mgumu. Tulikosa mwisho lakini tulitoa yote. Tutarejea katika mchezo wa marudiano Inshallah. Asante Bwana kwa bao na asisti. Utukufu wote ni wako. Mwanzo wa mambo makubwa zaidi yanayokuja,” Olunga alishukuru Mungu.

Katika mpambano huo mkali, Cristiano Ronaldo alifunga mabao mawili ya hali ya juu huku Al Nassr wakiendeleza rekodi yao nzuri katika Ligi ya Mabingwa ya AFC msimu huu hadi mechi tatu kwa ushindi wa msisimko.

Nahodha wa Ureno, Ronaldo alimpa matumaini kipa Salah Zakaria ambaye aliwasili katika uwanja huo, kwa kumalizia kwa umbali mrefu kwenye kona ya mbali ya wavu kutoka umbali mfupi baada ya dakika ya saa, kisha akapiga kwa ustadi sekunde kutoka kwa kona kali usiku ambao uliwatia wasiwasi Saudi. Wapinzani wa taji la Ligi ya Pro.