Haaland afurahia rafiki yake Sancho kuondoka Man Utd na kurudi Borrusia Dortmund

Nyota wa zamani wa Dortmund Haaland alifurahi sana kuona Sancho akirudi kwenye uwanja wake wa zamani ambapo atapata fursa ya kugundua fomu yake ya zamani.

Muhtasari

• Ten Hag alimwacha nje ya kikosi chake kwa pambano kali la Ligi Kuu ya Uingereza dhidi ya Arsenal kutokana na "uchezaji wake mzuri mazoezini".

Haaland na Sancho
Haaland na Sancho
Image: Facebook

Mshambuliaji nyota wa Manchester City, Erling Haaland, amefurahishwa na kuona Jadon Sancho akimaliza vita vyake vya Manchester United kwa kurejea Borussia Dortmund.

Sancho alijiunga na United mwaka 2021 kufuatia mkataba wa pauni milioni 73 na Dortmund ambapo alifurahia miaka minne lakini alishindwa kuiga uchezaji wake mzuri Old Trafford.

Winga huyo aliweza kufunga mabao 12 pekee na asisti 6 katika michezo 82 akiwa na Mashetani Wekundu hadi pale alipokabiliana na meneja Erik ten Hag mwezi Septemba ambapo aliondolewa kwenye kikosi cha kwanza.

Ten Hag alimwacha nje ya kikosi chake kwa pambano kali la Ligi Kuu ya Uingereza dhidi ya Arsenal kutokana na "uchezaji wake mzuri mazoezini".

Mchezaji huyo wa kimataifa wa Uingereza kisha akajibu kwenye mitandao ya kijamii akidai kuwa aligeuzwa kuwa "mbeba lawama" na mtaalamu huyo wa Uholanzi.

Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 23 hakuweza kupata njia ya kurejea kwenye kikosi cha kwanza na hiyo ilipelekea kurejea Dortmund kwa mkopo.

sancho
sancho

Nyota wa zamani wa Dortmund Haaland alifurahi sana kuona Sancho akirudi kwenye uwanja wake wa zamani ambapo atapata fursa ya kugundua fomu yake ya zamani.

Mshambulizi huyo nyota alikaa nchini Ujerumani kwa mwaka mmoja akicheza na nyota wa United, ambaye alifunga mabao 50 na kutoa asisti 64 katika mechi 137 alizocheza.

Naye mchezaji huyo wa kimataifa wa Norway alisherehekea hatua hiyo kwa kutumia mitandao ya kijamii na kushiriki picha ya Sancho akiwa amevaa tena shati la Dortmund.

Haaland alitoa maelezo yafuatayo kwenye Instagram: "mtanashati."