•Olympiacos imekuwa timu ya kwanza kutoka Ugiriki kushinda taji la Ulaya baada ya kuwashinda Fiorentina 1-0 kwenye fainali ya ligi ya Uefa Conference.
•Panathinaikos ndiyo klabu pekee kutoka Ugiriki iliyotinga fainali ya kombe la Ulaya iliposhindwa na Ajax mwaka wa 1971.
Olympiacos imekuwa klabu ya kwanza ya Ugiriki kushinda taji la Ulaya baada ya ushindi wa 1-0 dhidi ya Fiorentina kwenye fainali ya ligi ya Uefa Conference.
Mshambulizi wa Morocco, Ayoub El Kaabi alifunga bao la ushindi dakika ya 116 na kuwawezesha vijana wa Jose Luis Mendilibar kuweka historia katika uwanja wa nyumbani wa wapinzani wao AEK Athens.
Kabla ya mafanikio ya Olympiacos, Panathinaikos ndiyo klabu pekee kutoka Ugiriki iliyotinga fainali ya Uropa iliposhindwa na Ajax iliyoongozwa na Johan Cruyff katika uamuzi wa Kombe la Ulaya la 1971.
Mendilibar mwenye umri wa miaka 63 alikua meneja wa tatu wa timu ya Ugiriki msimu huu alipochukua mikoba mwezi Februari na sasa ana mataji mfululizo ya Uropa baada ya kushinda ligi ya Europa akiwa na Sevilla mwaka jana.
"Ni heshima kuwafanya watu hawa wote kuwa na furaha, ninahisi furaha na furaha kubwa kuwafanya watu wajisikie hivi na kujitolea kwao," Mendilibar alisema.
Waziri mkuu wa Ugiriki Kyriakos Mitsotakis alielezea furaha yake pia kupitia chapisho la mtandaoni :"Olympiacos imeshinda ligi ya mikutano ya Europa na kuweka historia! Usiku wa kusisimua kwa klabu yenyewe, lakini pia kwa soka la Ugiriki kwa ujumla.”
Kwa Fiorentina kilikuwa kipigo cha pili katika fainali ndani ya miezi 12 kufuatia kichapo cha mwisho cha msimu uliopita dhidi ya West Ham.