Mchezaji wa Spurs amwagiwa pilipili machoni na watu waliojifanya mashabiki kabla ya kumuibia

Taarifa zinadai kwamba mchezaji huyo alikuwa kwenye mitaa nchini Ufaransa kundi la watu waliojifanya kuwa mashabiki wake walipomkaribia wakimuomba kupigwa picha pamoja kabla ya kumtupia pilipili machoni na kutoweka na vitu vyake.

Muhtasari

• Kiungo huyo wa kati wa Spurs, 27, aliporwa saa yake ya kifahari ya Richard Mille yenye thamani ya pauni 260,000 [Zaidi ya shilingi za Kenya milioni 43] .

Yvis Bissouma
Yvis Bissouma

Nyota wa Tottnham Hotspurs, Yves Bissouma alishawishiwa na genge lililojifanya kama mashabiki wakitaka kujipiga picha pamoja na yeye kabla ya kupigwa mabomu ya machozi na kuibiwa, polisi wamefichua, kwa mujibu wa jarida la The Sun.

Kiungo huyo wa kati wa Spurs, 27, aliporwa saa yake ya kifahari ya Richard Mille yenye thamani ya pauni 260,000 [Zaidi ya shilingi za Kenya milioni 43] alipowasili katika hoteli moja ya Ufaransa akiwa na mpenzi wake asubuhi ya Jumapili.

Watu wawili waliojifunika nyuso zao pia waling'oa pete tatu za almasi kwenye vidole vya mpenzi wake ambaye hajatambuliwa walipokuwa wakijaribu kuingia katika hoteli ya nyota tano ya Majestic Barriere huko Cannes mwendo wa saa nne asubuhi.

Maafisa katika eneo la mapumziko la French Riviera walielezea jinsi wawili hao walivyokabiliwa na wahalifu hao, huku Bissouma akiwaambia polisi alijaribu kukimbilia ndani ya mali hiyo ya nyota tano - lakini milango yake ilikuwa imefungwa.

"Walikuwa ni sehemu ya genge lililopangwa vizuri," chanzo cha polisi wa mahakama kilisema.

"Wote wawili walikuwa wakingoja nje ya hoteli hiyo, na waligongwa wakati wanandoa hao walipoangushwa na gari la abiria lililokuwa likiendeshwa na dereva mwendo wa saa nne asubuhi.

"Mwanzoni wanaume hao walifanya kama wanataka kupiga picha na nyota huyo, lakini ikawa wazi walikuwa wamevaa vinyago.

"Wanandoa hao walijaribu kuingia ndani ya hoteli hiyo, lakini walikabiliwa na mlango uliokuwa umefungwa, kisha gesi ikanyunyiziwa usoni mwao.

"Saa ya Richard Mille ilichukuliwa, pamoja na pete tatu za almasi, kabla ya watu hao kutoroka kwa kutumia Renault Megane."

Bissouma na mpenzi wake walishtushwa na kufadhaishwa sana na shambulio hilo hivi kwamba walirudi London ndani ya masaa machache