logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Euro 2024: England yaanza kampeni kwa ushindi wa 1-0 dhidi ya Serbia

kiwango chao kilichopungua kikiruhusu Serbia kutumia vizuri shinikizo hiyo.

image

Michezo17 June 2024 - 06:33

Muhtasari


  • Msimu mzuri wa Bellingham - ambao ulimletea ushindi wa Ligi ya Mabingwa mwishoni mwa kampeni yake ya kwanza akiwa na Real Madrid - uliendelea huku akionyesha hasa kwa nini anachukuliwa kuwa supastaa mpya wa Uingereza.

Jude Bellingham aliiwezesha Uingereza kuanza kwa michuano ya Euro 2024 kwa bao la ushindi na uchezaji mzuri katika ushindi wao dhidi Serbia mjini Gelsenkirchen.

Msimu mzuri wa Bellingham - ambao ulimletea ushindi wa Ligi ya Mabingwa mwishoni mwa kampeni yake ya kwanza akiwa na Real Madrid - uliendelea huku akionyesha hasa kwa nini anachukuliwa kuwa supastaa mpya wa Uingereza.

England, ambao walianza na beki wa pembeni wa Liverpool, Trent Alexander-Arnold katika safu ya kati, walirudi katika mazoea ya zamani baada ya mapumziko wakiwa wamekaa nyuma, kiwango chao kilichopungua kikiruhusu Serbia kutumia vizuri shinikizo hiyo. Kipa Jordan Pickford aliokoa mkwaju katika dakika za lala salama kutoka kwa Dusan Vlahovic.

Harry Kane alikaribia kuongeza bao la pili kwa England wakati mpira wa kichwa kutoka kwa Jarrod Bowen ulipogonga lango na kuokolewa na kipa wa Serbia Predrag Rajkovic.

England itahitaji kuimarika, lakini haya yalikuwa angalau matokeo yatakayowapeleka kwenye mchezo wao wa pili wa Kundi C dhidi ya Denmark siku ya Alhamisi wakiwa na matumaini

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved