logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Sajili mpya wa Chelsea Kiernan Dewsbury-Hall: Nafuata nyayo za Lampard na Kante

"Ni dhahiri kwamba ninamjua kocha na jinsi anatutaka tucheze na pia kukosi hiki kimejaa talanta tupu."

image
na Davis Ojiambo

Michezo03 July 2024 - 09:37

Muhtasari


  • • "Ni dhahiri kwamba ninamjua kocha na jinsi anatutaka tucheze na pia kukosi hiki kimejaa talanta tupu."
  •  
Kiernan Dewsbury-Hall

Mchezaji sajili mpya wa miamba wa London, Chelsea, Kiernan Dewsbury-Hall amefunguka kuhusu ndoto yake ya utotoni na jinsi baadhi ya wachezaji wa awali wa Chelsea walivyomvutia kwenye soka. 

Akizungumza na waandishi wa habari wa Chelsea siku moja baada ya utambulisho klabuni humo, Dewsbury-Hall alisema kwamba tangu utotoni, amekua akifuatilia uchezaji wa viungo wa kati wa Chelsea waliofana enzi zao.

Pia alisema kulichomvutia kuikataa Brighton na kuichagua Chelsea ni ukaribu wake ba kocha mpya wa Chelsea, Enzo Maresca.

"Ni dhahiri kwamba ninamjua kocha na jinsi anatutaka tucheze na pia kukosi hiki kimejaa talanta tupu."

"Kuna wachezaji wengi wazuri ambao nimekuwa nikiwatazama tangu utotoni. Wa kwanza kabisa ni Frank Lampard, kiungo wa kati aliyezoea kufunga mabao; kitu ambacho ningependa kujaribu na kuifanya kuwa moja ya uchezaji wangu..."

"...lakini pia wachezaji kama Fabregas, Mata na hata Kante ambaye tulikuwa na yeye Leicester City " Dewsbury-Hall alisem.

Chelsea walimsajili Dewsbury-Hall kutoka Leicester kwa kitita cha pauni milioni 30 na kutia saini mkataba wa miaka 5 na Chaguo la mwaka mmoja zaidi.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved