Kinda Lamine Yamal avunja rekodi ya Pele wa Brazil iliyodumu kwa miaka 66

Yamal amekuwa mchezaji mchanga zaidi kuwahi kufunga bao katika nusu fainali ya kipute cha Euro au kombe la dunia, na kuisambaratisha rekodi hiyo iliyokuwa imeshikiliwa na marehemu Pele kwa miaka 66.

Muhtasari

• Ufaransa walipata bao la kuongoza dakika ya nane kupitia kwa Randal Kolo Muani akiunganisha kwa kichwa pasi na Kylian Mbappe.

• Winga huyo wa Barcelona alimkejeli Andrian Rabiot kabla ya kutoa kombora kali la kona ya juu kutoka nje ya eneo la hatari kwa 1-1.

Kinda wa Barcelona na timu ya taifa ya Uhispania, Lamine Yamal mwenye umri wa miaka 16 amevunja rekodi ya mkongwe wa Brazil, Pele baada ya kufunga bao muhimu la kuipeleka Uhispania kwenye fainali ya kipute cha Euro 2024.

Yamal amekuwa mchezaji mchanga zaidi kuwahi kufunga bao katika nusu fainali ya kipute cha Euro au kombe la dunia, na kuisambaratisha rekodi hiyo iliyokuwa imeshikiliwa na marehemu Pele kwa miaka 66.

Shuti la Lamine Yamal kutoka umbali wa mita 25 na mkwaju wa Dani Olmo uliisaidia Uhispania kushinda nakisi ya mabao na kuishinda Ufaransa katika nusu-fainali kwenye Uwanja wa Allianz Arena Jumanne.

Ufaransa walipata bao la kuongoza dakika ya nane kupitia kwa Randal Kolo Muani akiunganisha kwa kichwa pasi na Kylian Mbappe.

Winga huyo wa Barcelona alimkejeli Andrian Rabiot kabla ya kutoa kombora kali la kona ya juu kutoka nje ya eneo la hatari kwa 1-1.

Bao hilo linamfanya kijana huyo mwenye umri wa miaka 16 kuwa mfungaji mwenye umri mdogo zaidi katika historia ya michuano ya Ulaya.

Olmo aliiweka Uhispania bao la kuongoza dakika nne baadaye, akimkwepa Aurelien Tchouameni kabla ya kombora lake kuingia langoni mwa wavu kwa mabao 2-1 licha ya juhudi bora za Jules Kounde.

Pande zote mbili ziliendelea kutishana baada ya muda, lakini Ufaransa haikuweza kupata njia licha ya kumtambulisha Olivier Giroud, mfungaji bora wa muda wote wa nchi hiyo.

Hata hivyo, kikosi cha Luis de la Fuente cha La Roja kiliweza kucheza vyema zaidi katika hatua za mwisho, na kuwaondoa Ufaransa kwenye michuano hiyo na kutinga fainali yao ya kwanza ya Euro tangu 2012.