logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Libya yaadhibiwa na shirikisho la soka barani Africa CAF

Shirikisho la soka la Libya limetakiwa kulipa faini ya shilingi 6.45M

image
na Brandon Asiema

Football27 October 2024 - 08:45

Muhtasari


  • Nigeria imekabidhiwa alama 3 na pointi 3 baada ya mechi hiyo kufutiliwa mbali na bodi ya nidhamu ya CAF






Shirikisho la soka barani Afrika CAF kupitia bodi ya nidhamu imeaidhibu timu ya taifa la Libya baada ya mahangaiko iliyopitia timu ya Nigeria nchini Libya.


Kupitia ujumbe kwa vyombo vya habari, bodi hiyo ya nidhamu baada ya kufanuya uchunguzi iliipata Libya na makossa ya kukiuka vifungu vya 31, 82 na 151 vya sheria vya CAF.


Mataifa hayo mawili yalifaa kucheza mechi za kufuzu kombe ya mataifa barani Afrika AFCON mnamo tarehe 15 October lakini mechi ilihairishwa kutokana na upokezi mbovu wa timu ya Nigeria katika uwanja wa ndege nchini Libya.


Kutokana na hatia, Nigeria wamefaidi magoli matatu na alama tatu baada ya mechi hiyo kufutiliwa mbali na CAF.


Vile vile, shirikisho la soka la nchi ya Libya, limepigwa faini ya dola elfu hamsini na imetakiwa kulipa faini hiyo chini ya siku sitini baada ya kutaarifiwa na CAF.



RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved