logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Harambee Stars wanamatumaini ya kufika katika fainali ya kombe la Mapinduzi

Harambee Stars kwa sasa wanashikilia nafasi ya kwanza na pointi 4 huku Burkina Faso wakifuata kwa ukaribu na pointi 4 .

image
na OTIENO TONNY

Football09 January 2025 - 10:53

Muhtasari


  • Kati ya mechi mbili ambazo zimegaragazwa tayari timu ya Kenya imepata ushindi katika mechi moja na kuenda sare katika moja vilevile.
  • Mechi hiyo kati ya Kenya na Zanzibar itaamua hatma ya Kenya kwani wanahitaji ushindi au sare ili kufuzu  fainali.


Timu ya soka ya Kenya Harambee Stars wanamatumaini ya kufika katika fainali ya kinyang’anyiro ya kombe la Mapinduzi. Stars wanahitaji matokeo ya sare katika mechi yao ya mwisho katika kikundu dhidi ya wenyeji wa mashindano hayo  Zanzibar .

Iwapo mchuano huo ambapo utakaragazwa katika uga wa Gombani Ijumaa kuanzia saa moja jioni  itaishia  sare basi Harambee stars watafuzu moja kwa moja hadi katika fainali ya kombe la Mapinduzi.

Harambee Stars kwa sasa wanashikilia nafasi ya kwanza na pointi 4 huku Burkina Faso wanafuata kwa karibu na pointi 4 huku Kenya wakiwa mbele na idadi ya mabao, Timu ya Zanziba wanashikilia nafasi ya tatu na pointi tatu huku Tanzania wakishikilia nafasi ya mwisho ikiwa hawajaandikisha pointi yeyote.

Kati ya mechi mbili ambazo zimekaragazwa tayari timu ya Kenya imetua ushindi katika mechi moja waliocheza dhidi ya Tanzania walipoilaza mabao mawili kwa nunge na kuenda sare ya bao moja na timu ya Bukina Faso.

Mechi hiyo kati ya Kenya na Zanzibar itaamua hatma ya Kenya kwani wanahitaji ushindi au sare ili kufuzu  fainali .

Timu mbili ambazo zitamaliza katika nafasi ya kwanza na ya pili mtawalia zitafuzu kushiriki fainali ambayo imeratibiwa kukaragazwa tarehe 13, January

Michuano ya Mapinduzi Cup inaipa Kenya fursa nzuri ya kufanya maandalizi mazuri kabla ya michuano ijayo ya CHAN, ambayo itaandaliwa nchi tatu za Africa Mashariki ikiwemo Kenya, Uganda na Tanzania baadaye mwaka huu.



RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved