logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Real Madrid Kuchuana na Barcelona katika fainali ya Spanish Super Cup

Mabingwa wa Uhispania Real Madrid walipata ushindi ya mabao matatu kwa sufuri dhidi ya Mallorca.

image
na OTIENO TONNY

Football10 January 2025 - 09:25

Muhtasari


  • Real Madrid iliicharaza timu ya Malloca siku ya Alhamisi katika nusu fainali mabao matatu kwa sufuri.
  • Jude Bellingham na Rodrygo walipachika mabao na kuipa Real Madrid ushindi  uliowawezesha kufuzu kushiriki fainali na wapinzani wao wakuu Barcelona.


Mabingwa wa Uhispania Real Madrid watachuana na Barcelona katika fainali ya Spanish Super Cup Jumapili tarehe 12, January 2025.

Real Madrid iliicharaza timu ya Malloca siku ya Alhamisi katika nusu fainali mabao matatu kwa sufuri huku awali Barcelona iliicharaza Athletic Bilbao mabao mawili kwa sufuri na  kuwapa nafasi ya  kufuzu moja kwa moja kwa fainali ya Spanish Super Cup.

Jude Bellingham na Rodrygo walipachika mabao na kuipa Real Madrid ushindi  uliowawezesha kufuzu kushiriki fainali na wapinzani wao wa jadi  Barcelona.

Madrid wana nafasi ya kulipiza kisasi kwa kushindwa kwao kwa Clasico katika La Liga mwezi Oktoba 2024, ambapo Barcelona ilipata ushindi wa 4-0 dhidi yao.

Mashabiki wa Madrid walijaza uga wa Jeddah kuishabikia timu yao ambayo ilionekana kutumia vizuri nafasi walizozipata kwa faida yao huku bao la kujifunga lake Valjent likifanikisha ushindi pamoja na bao la tatu kutoka kwa mchezaji Rodrygo katika dakika za lala salama.

Wapenzi wa soka sasa wanatarajia kushuhudia fainali hiyo ambayo itachezwa  katika uga wa King Abdullah Sports City.


 



RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved