logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Lisandro Martinez aandika ujumbe wa hisia baada ya upasuaji kufuatia jeraha

Kufikia sasa Martinez ameshinda mataji mawili na Manchester United yote yakiwa ya FA.

image
na Japheth Nyongesa

Football17 February 2025 - 11:50

Muhtasari


  • Muargentina huyo alipata jeraha katika mchuano wa  hivi karibuni  Man United  2-0 dhidi ya Crystal Palace katika uwanja wa Old Trafford na huenda akakosa mechi zote zilizosaliasalia za mwaka wa kalenda.
  • Lisandro Martínez mwenye umri wa miaka 27 alijiunga na Manchester United mnamo Julai 2022, akiungana tena na meneja wa zamani wa Ajax Erik ten Hag. Beki huyo wa Argentina alisajiliwa kwa ada ya karibu £57 milioni.

Beki wa Manchester United Lisandro Martinez amechapisha ujumbe kwa wanasoka wenzake wa timu hiyo baada ya kufanyiwa upasuaji kutoka na jeraha lake alilopata kwenye mchuano dhidi ya Crystal Palace.

Muargentina huyo alipata jeraha katika mchuano ambao walishinda 2 - 0 katika uwanja wa Old Trafford. Duru zinaarifu kwamba huenda akakosa mechi zote zilizosaliasalia katika mwaka wa kalenda msimu huu.

'Ninahisi shukrani kubwa kwa kazi nzuri na msaada wa Man Utd, shirikisho la soka Argentina, familia yangu, marafiki, wachezaji wenzangu, na kila mtu aliyechukua muda kunitumia ujumbe wa kutia moyo. Upasuaji ulienda vizuri! Sasa ni wakati wa kutoa juhudo zangu, kwa moyo na roho, katika mchakato wa ukarabati," alieleza.

Martinez amekosa mechi zaidi ya 50 tangu ajiunge na United kutokana na jeraha, ingawa kurudi kwake hivi karibuni ni muhimu.

Martinez amekuwa mmoja wa wachezaji bora wa United tangu Ruben Amorim alipochukua mikoba ya Mashetani Wekundu mwezi Novemba, akifunga bao muhimu sana katika uwanja wa Anfield wakati United ilipochukua pointi moja dhidi ya wapinzani wao Liverpool mwanzoni mwa mwaka huu.

Akiandika kwenye Instagram, Martinez aliandika: "Leo, baada ya kupita siku kadhaa ngumu ambapo nilijiruhusu kuhisi na kukubali huzuni yangu, kutokuwa na msaada, kutokuwa na usalama, hofu, na usawa wa kihisia, ninaunganisha tena na kiini changu na maadili yangu, ambayo hunisaidia kuona vitu kutoka kwa mtazamo mzuri na mzuri zaidi,"

Beki huyo wa kati, aliyepewa jina la utani " The Butcher" kwa sababu ya mtindo wake wa kucheza, ni mmoja wa wachezaji kadhaa ambao kwa sasa wako katika chumba cha matibabu cha United - Amad Diallo, Manuel Ugarte, Kobbie Mainoo na Toby Collyer wote wamepata majeraha hivi karibuni

Kufikia sasa Martinez ameshinda mataji mawili na Manchester United yote yakiwa ya FA.

Lisandro Martínez mwenye umri wa miaka 27 alijiunga na Manchester United mnamo Julai 2022, akiungana tena na meneja wa zamani wa Ajax Erik ten Hag. Beki huyo wa Argentina alisajiliwa kwa ada ya karibu £57 milioni, na kuwa moja ya usajili wa juu zaidi wa dirisha la kwanza la uhamisho la meneja wa zamani wa Manchester United Erick Ten Hag.



RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved