Mwamuzi wa katikati mwa uwanja Munuera Montero sasa hatakuwa mwamuzi wa michuano kwa muda usiojulikana kutokana na kupewa likizo ya lazima kutoa kwa ligii kuu ya La Liga na vile vile ligii kuu ya mabingwa ulaya ' UEFA'.
Hili hasa huenda limechangiwa pakubwa na kadi nyekundu aliyotoa kwa Jude Bellingham wa Real Madrid kwenye mchuano wao dhidi ya Osasuna.
Maamuzi hayo yamechukua hatua ambayo haikutarajiwa, - mwamuzi Jose Luis Munuera Montero - sasa anachunguzwa na RFEF.
Afisa huyo, ambaye alitoa kadi nyekundu moja kwa moja kwa wapinzani, sasa anakabiliwa na uwezekano wa marufuku kubwa kutokana na "mgogoro wa maslahi."
Kuchanganyikiwa kwa Bellingham kuliibuka wakati wa sare ya 1-1 ya Real Madrid na Osasuna, kamera zilionekana kumshika akimwambia Munuera Montero, "Ninazungumza nawe kwa heshima,"
Hata hivyo, mchezaji huyo nyota wa Uingereza mwenye umri wa miaka 21 tangu wakati huo amesisitiza kuwa "hakuwahi kumtukana mwamuzi," akidai kuwa matamshi yake yalikuwa "kielelezo kwangu."
Meneja wa Real Madrid Carlo Ancelotti pia amemuunga mkono mchezaji wake, akisisitiza kuwa hali nzima ilikuwa kutokuelewana.
Bellingham aliachwa kwa mshangao wakati mwamuzi Montero alipotoa kadi nyekundu katika kipindi cha kwanza cha mechi ya Real Madrid dhidi ya Osasuna katika LaLiga, huku ikiripotiwa kuwa afisa huyo alisema 'f *** you'.
Nyota huyo wa Los Blancos anaweza kukabiliwa na marufuku ya mechi 12 kwa tukio hilo, ambalo limeshuhudia Bellingham akitetewa kwa shauku na kocha wake mkuu Carlo Ancelotti.
Pia imeripotiwa kwamba tangu tukio hilo Madrid imedhaniwa kukasirishwa dhidi ya uamuzi huo kwa muchezaji wao, hivyo mabigwa hao wametishia kuondoka kwenye ligii hiyo ya Uhisipania.
Baada ya tukio hilo, ambalo liliifanya Madrid kupunguzwa hadi wachezaji 10 na kulazimika kucheza zaidi ya nusu ya mchezo huo wakiwa wachezaji tisa na kutoka sare ya 1-1 na kupoteza nafasi katika mbio za ubingwa - Munera Montero alikabiliwa na vitisho vya kuuawa.
Katika tukio lisilohusiana, amejikuta akichunguzwa na kamati ya Shirikisho la Soka la Uhispania.
Kwa upande wake mwamuzi huyo wa FIFA tangu 2019 amejitenga na uchunguzi huo akiamini hana hatia.
"Hatimaye, natarajia kwamba nitajieleza na ushahidi wangu dhidi ya vyombo vya habari ambavyo kwa makusudi au bila ya huruma vimesambaza uongo, habari zisizo sahihi na za upendeleo, na kusababisha uharibifu usioweza kurekebishwa kwa heshima ya kitaaluma, sifa yangu mwenyewe, kikundi cha waamuzi pamoja na faragha yangu binafsi na ile ya watu wengine."