Mmiliki wa asilimia kubwa ya hisa katika timu ya Manchester united inayoshiriki ligii kuu ya uingereza Sir Jim Ratcliffe amesema kwamba ana matumaini ya kujenga mojawapo ya viwanja vizuri zaidi duniani.
Mmiliki huyo akizungumza kwenye mahojiano na wanahabari pia amekiri kwamba kwa sasa timu hiyo ina changamoto za kifedha lakini wako tayari kupigana na changamoto hiyo.
Vilevile amefichua kwamba huenda akatafuta usaidizi wa serikali ya uingereza kumusaidia ili kufanikisha lengo lake kwa timu hiyo ya manchesater United.
'Kama itaendelea, basi, nadhani, tunaunga mkono hilo kwa uwanja mpya. Kwa sababu ya miradi ya kuongeza mwanga unahitaji kiini, unahitaji moyo kwa mpango, vinginevyo ni mali ya makazi tu. Lakini nadhani kama tungejenga uwanja wa mpira wa miguu wa kisasa zaidi duniani, ambao nadhani tutaufanya, basi hilo litavutia mashabiki bilioni ambao tumewapata duniani kote. Wote wanataka kwenda Manchester," alisema Ratcliffe.
Wakati huo ameongeza kwamba pesa sio changamoto lakini ataona cha kufanya na kuahidi kuzungumzia hilo jambo hivi karibuni. "Fedha sio suala, nadhani suala si la kifedha sana. Lakini maelezo ya kina ya kwamba tunataka kuzungumza juu ya hiyo siku zijazo. Itakuwa ya kuhusu kifedha, nadhani," alieleza.
Mmiliki huyo wa Manchester united hata hivyo amekiri kuwepo na changamoto za kifedha hasa kwa matumizi ya timu, akitaja hilo kama linalochangiwa na matokea yasiyomazuri kwa timu ya manchester United.
"Ni suala rahisi. Kama unatumia zaidi ya wewe kupata hatimaye hiyo ni njia ya uharibifu. Kwa misimu saba iliyopita, ikiwa utajumuisha msimu huu, klabu ingekuwa imepoteza pesa. misimu saba mfululizo. Nadhani hiyo ni jumla ya £330m, hivyo karibu theluthi moja ya fedha bilioni ambazo zimetoka nje ya klabu katika misimu minne au mitano iliyopita," alisema.
"Gharama za kuendesha klabu hiyo katika miaka saba iliyopita zimeongezeka kwa £100m. Gharama ya bili ya mshahara wa wachezaji katika miaka saba iliyopita au hivyo ni £ 100m. Ongezeko la mapato katika kipindi hicho ni £100m. Na kiasi hicho hakifanyi kazi. Kama unapoteza pesa kila mwaka, na wakati huo huo unaongeza gharama zako za kuendesha klabu, haifanyi kazi na inaishia katika shida. Na hapo ndipo klabu hii ingemaliza mwishoni mwa mwaka huu," alieleza mmiliki huyo akieleza kuhusu maamuzu ya timu hiyo ya mashetani wekungu kupunguza matumizi ya Fedha.