logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Klabu ya Chelsea yanunua Kinda wawili kutoka Sporting Lisbon ya Portugal

Chelsea wanaendelea na sera yao kali ya kuajiri huku wakishinikiza kufuzu kwa Ligi ya Mabingwa.

image
na Japheth Nyongesa

Football21 March 2025 - 11:00

Muhtasari


  • Klabu hiyo ya Ureno ilithibitisha rasmi uhamisho huo Jumatano usiku.
  • Quenda, ambaye alikuwa akihusishwa na Manchester United na meneja wa zamani Ruben Amorim, atasalia Sporting hadi mwisho wa msimu ujao kabla ya kujiunga na Chelsea.

Dario Essugo, chelsea new player from sporting Lisbon
Chelsea wamefanikiwa kukamilisha usajili wa Geovany Quenda na Dario Essugo kutoka Sporting Lisbon katika mkataba wenye thamani ya takriban pauni milioni 62.5 (dola milioni 81)

Klabu hiyo ya Ureno ilithibitisha rasmi uhamisho huo Jumatano usiku, ikifichua kuwa winga Quenda mwenye umri wa miaka 17 alinunuliwa kwa karibu pauni milioni 44, huku kiungo wa ulinzi Essugo, 20, akisainiwa kwa pauni milioni 18.5.

Quenda, ambaye alikuwa akihusishwa na Manchester United na meneja wa zamani Ruben Amorim, atasalia Sporting hadi mwisho wa msimu ujao kabla ya kujiunga na Chelsea.

Wakati huo huo, Essugo atamaliza kampeni ya sasa kwa mkopo katika klabu ya La Liga Las Palmas kabla ya kuhamia  London msimu ujao.

Ununuzi huo unalingana na mkakati wa Chelsea wa kuwekeza katika vipaji vya vijana, kufuatia hatua kama hizo kwa watoto wa miaka 17 Estevao Willian na Kendry Paez, ambao wanatarajiwa kuwasili msimu ujao.

Quenda tayari amejitambulisha katika kikosi cha kwanza cha Sporting, akicheza kwa mara ya kwanza Ligi ya Mabingwa mnamo Septemba na kufunga bao lake la kwanza la ligi mnamo Oktoba dhidi ya Famalicao.

Essugo, anayejulikana kwa uwepo wake mkubwa wa ulinzi, anaweza anaweza kucheza viizuri katika safu ya kiungo, uwezekano wa kutumika kama msaidizi wa Moises Caicedo.

Chelsea, chini ya umiliki wa Todd Boehly na Clearlake Capital, wanaendelea na sera yao kali ya kuajiri huku wakishinikiza kufuzu kwa Ligi ya Mabingwa, kwa sasa wanashika nafasi ya nne kwenye msimamo wa Ligi Kuu.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved