logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Gor Mahia yamjibu kocha Benn McCarthy kuhusu madai ya kutowaachilia wachezaji

McCarthy alituhumu klabu ya Gor Mahia na Tusker FC kwa kushindwa kuwaachilia wachezaji wao.

image
na Japheth Nyongesa

Football24 March 2025 - 15:00

Muhtasari


  • Oruo alitetea msimamo wa klabu, akisisitiza kuwa walifuata kanuni za kuachilia wachezaji kwa ajili ya majukumu ya kimataifa.
  • "Wachezaji waliopatikana wakati huo ndio niliowachagua. Gor Mahia na Tusker waliomba ruhusa ya kuwabakisha wachezaji wao, na tulikubaliana.," Alisema MacCarthy
Gori Mahia FC
Baada ya mechi ya Harambee Stars  dhidi ya Gabon kukamilika na kenya kupoteza 2- 1 mikononi mwa wageni, Mkufunzi mkuu wa timu ya taifa Benn MacCarthy alizungumzia hali hiyo na kueleza mchakato wa maamuzi yake ya kuchagua wachezaji.

McCarthy alituhumu klabu ya Gor Mahia na Tusker FC  kwa kukosa kuwaachilia wachezaji wao kwa ajili ya mechi za kufuzu Kombe la Dunia dhidi ya Gambia na Gabon.

Klabu ya soka ya Gor Mahia imetoa majibu kufuatia madai hayo yaliyotolewa na kocha mkuu wa Harambee Stars kupitia mkurugenzi mtendaji Raymond Oruo imejitenga na kauli hiyo. 

Katika majibu yake, Oruo alitetea msimamo wa klabu, akisisitiza kuwa walifuata kanuni za kuachilia wachezaji kwa ajili ya majukumu ya kimataifa.

Vilevile alieleza kuwa klabu ilifuata taratibu zote kwa mujibu wa sheria, na wachezaji wao waliungana na timu ya taifa mara tu baada ya mechi yao dhidi ya Bandari kukamilika.

"Nimeona taarifa ya kocha mkuu wa Harambee Stars baada ya mechi dhidi ya Gabon. Kocha na FKF wanajua vyema kanuni zinazohusu kuachilia wachezaji kwa majukumu ya kimataifa. Klabu zetu hazipaswi kutendewa kwa njia tofauti," Oruo alieleza.

Aliongeza kuwa kocha alipata fursa ya kuwafuatilia wachezaji wa Gor Mahia katika mechi ya ushindani dhidi ya Kariobangi Sharks na alipaswa kufanya maamuzi yake kulingana na hilo.

"Wachezaji wetu walikuwa tayari mara tu baada ya mechi dhidi ya Bandari. Ikiwa kocha aliamua kuwa hawahitajiki kwenye kikosi chake, basi anapaswa kusema hivyo wazi kwani alikuwa na nafasi ya kuwaona katika mechi ya ligi," aliongeza.

Oruo alihitimisha kwa kusisitiza kuwa Gor Mahia itaendelea kuunga mkono juhudi za timu ya taifa, "Klabu itaendelea kusaidia jitihada za timu ya taifa." alisema.

Kocha mkuu wa timu ya taifa Harambee Stars McCarthy alikua amesema kwamba vilabu vya Gori Mahia na Tusker walikuwa wameomba kubakisha wachezaji wao na walikubalina kuhusu hilo. 

"Wachezaji waliopatikana wakati huo ndio niliowachagua. Gor Mahia na Tusker waliomba ruhusa ya kuwabakisha wachezaji wao, na tulikubaliana. Lakini siwezi kuchagua wachezaji ambao sijawaona wakicheza au ambao siwajui, ndiyo maana hakuna aliyekuwa kwenye kikosi," McCarthy alisema baada ya mechi ya Jumapili.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved