logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Kiungo William Lenkupae afichua kilichomfanya achague kuwakilisha Kenya badala ya Australia

Lenkupae, amefichua sababu iliyomfanya achague kuiwakilisha Kenya badala ya Australia.

image
na Japheth Nyongesa

Football24 March 2025 - 11:47

Muhtasari


  • Willson Lenkupae alizaliwa Australia akiwa na asili ya wakenya kutoka kabila la Samburu.
  • Alichagua kuwakilisha Kenya badala ya Australia.

William Willson Lenkupae
Kiungo wa Harambee Stars, William Wilson Lenkupae, amefichua sababu iliyomfanya achague kuiwakilisha Kenya badala ya Australia, taifa lake lingine.

Mwanasoka huyo alieleza kwamba kilichomchochea zaidi ni kutokana na sababu kwamba familia yake kubwa iko hapa kenya na amekuwa na uhusiano wa karibu na taifa la Kenya.

“Ilikuwa wazo zuri kichwani mwangu, na nilihisi huu ulikuwa wakati mwafaka kwangu. Nimekuwa na uhusiano wa karibu na Kenya kila wakati. Baba yangu yupo hapa, mjomba wangu yupo hapa, familia yangu ipo hapa, kwa hivyo daima nimekuwa na mshikamano na nchi hii," alieleza Lenkupae.

"Pia nilijua kwamba hii ni timu nzuri ambayo ningependa kuwa sehemu yake, na ninashukuru kuwa sehemu yake kwa sasa," alisema Lenkupae.
Mwanasoka huyo pia alionesha furaha zaidi kwa kuiwakilisha kenya. Aliongeza kwamba familia zake zote kwa mataifa haya mawili, Kenya na Australia wote walifurahia maamuzi yake.
"Ni mafanikio makubwa na ndoto iliyotimia, kusema kweli. Familia yangu nchini Australia ilikuwa na furaha sana, kama ilivyokuwa familia yangu hapa Kenya. Ni mafanikio makubwa na kumbukumbu ya thamani nitakayobeba hadi Australia," aliongeza.

Willson Lenkupae alizaliwa Australia akiwa na asili ya wakenya kutoka kabila la Samburu, alichagua kuwakilisha Kenya badala ya Australia.

Alipokea mwito wake wa kwanza wa kimataifa katika timu ya taifa ya Kenya mnamo Machi 2025 kwa mechi zao za kufuzu kwa Kombe la Dunia la 2026 dhidi ya Gambia na Gabon. Mnamo tarehe 20 Machi, alifunga bao lake la kwanza katika sare ya mabao 3 dhidi ya Gambia.

William Lenkupae aliyezaliwa 23 Disemba 2001 ni mchezaji wa soka wa Kenya ambaye anacheza kama kiungo wa katika klabu ya Central Coast Mariners ya Australia na timu ya taifa ya Kenya.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved