logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Patrick Matasi asimamishwa kutoshiriki soka kwa siku 90

Shirikisho la FKF likitoa uamuzi huo limerejelea video ambayo imesambazwa mitandao.

image
na Japheth Nyongesa

Football28 March 2025 - 08:20

Muhtasari


  •  Usimamizi wa shirika hilo limeeleza kwamba maamuzi hayo yako ni sahihi kulingana na sheria za michezo nchini.
  • "FKF itashirikiana na FIFA, CAF na mamlaka mengine husika. Uchunguzi umeanzishwa kuhusu hilo swala.

Patrick Matasi
Mlinda lango wa timu ya taifa ya Kenya na Harambee Stars na vile vile klambu ya kandanda ya Kakamega Home Boys Patrick Matasi amesimamishwa kwa muda wa siku 90 kutoshiriki katika soka la kulipwa.

Shirikisho la soka nchini Kenya FKF, likitoa uamuzi huo limerejelea video ambayo imesambazwa mitandao ikimuhusisha mwanasoka huyo na madai ya ubadhirifu wa michezo ambayo ni hatia kubwa kwa wanasoka wote duniani.

FKF kwenye barua iliofikia sitesheni ya Radio Jambo imetoa tangazo kwamba mchezaji huyo atakua inje ya soka la kulipwa kwa siku 90 huku uchunguzi ukiendela kufanyika. Usimamizi wa shirika hilo limeeleza kwamba maamuzi hayo yako ni sahihi kulingana na sheria za michezo nchini.

"Shirikisho la soka nchini Kenya [FKF] limempa likizo ya muda mlinda lango Patrick Matasi kutoshiriki kwa shughuli zote ambazo zipo chini ya FKF kwa muda wa siku 90.  Maamuzi haya yanatokana na video ambayo inasambaa inayoonesha uwezekano wa kuiuka kwa sheria za michezo," barua ilisomeka.

"Maamuzi haya yamefanyika kulingana na sheria kifungu VII [2] ya FKF ya ukiukaji wa sheria za michezo ya mwaka 2016. Hili limefikishwa kwa timu ya soka ya Kakamega Homeboys na mchezaji husika," barua iliendelea.

Wakati huo huo shirikisho la FKF pia limesema kwamba liotahusisha mamlaka tofauti tofauti ilikiwa ni pamoja mashirikisho mengine ya soka kama vile FIFA na CAF ili kuhakikisha uchunguzi wa wazi kwa wahusika wote.

"FKF itashirikiana na FIFA, CAF na mamlaka mengine husika. Uchunguzi umeanzishwa kuhusu hilo swala. Shirikisho litasailia wazi kushikilia viwango vya soka nchinina kuhakikisha kuna uwazi wa kutosha kwa sehemu zote husika,' barua hiyo ilisomeka zaidi.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved