Tazama walioteuliwa kuwania Ballon d'Or 2024, Ronaldo na Messi watemwa nje mara ya 1 tangu 2003

Wachezaji 30 wameteuiwa kuwania tuzo hilo la kifahari mwaka huu.

Muhtasari

•Baada ya msimu wa kukumbukwa wa 2023-24, orodha fupi ya walioteuliwa kuwania tuzo hilo la kifahari mwaka wa 2024 imetangazwa.

•Ni vizuri kuona majina mapya katika orodha hiyo baada ya miongo 2 ya utawala wa Cristiano Ronaldo na Lionel Messi, ambao wote sasa wako nje ya orodha.

Image: HISANI

Orodha ya walioteuliwa kuwania tuzo ya mchezaji binafsi ya kifahari zaidi duniani, Ballon d’Or, imefichuliwa kabla ya hafla ya tuzo kufanyika mjini Paris, Ufaransa mnamo Oktoba 28, 2024.

Ballon d'Or bila shaka ndiyo tuzo ambayo kila mwanasoka duniani ana ndoto ya kushinda siku moja. Baada ya msimu wa kukumbukwa wa 2023-24, orodha fupi ya walioteuliwa kuwania tuzo hilo la kifahari mwaka wa 2024 imetangazwa.

Kuna baadhi ya wanasoka mahiri wanaowania kutwaa tuzo hiyo ambayo Lionel Messi alitwaa kwa mara ya nane mwaka 2023, huku matokeo si tu katika ngazi ya vilabu, bali pia katika michuano mbalimbali mikubwa iliyofanyika katika kipindi cha miezi 12 iliyopita, yakizingatia wakati wa kuchagua orodha ya mwaka huu ya washindi wanaotarajiwa.

Wachezaji wawili wa Real Madrid, Jude Bellingham na Vinicius Junior wamependekezwa sana kushinda tuzo hilo, huku wawili hao wakiwa na mafanikio mengi msimu uliopita.

Erling Haaland, Phil Foden, Nico Williams na Lamine Yamal wote pia watakuwa miongoni mwa wale wanaotarajia kumaliza katika nafasi bora kwenye tuzo hizo.

Ni vizuri kuona baadhi ya majina mapya katika orodha hiyo baada ya miongo miwili ya utawala wa Cristiano Ronaldo na Lionel Messi, ambao wote sasa wako nje ya orodha.

Tazama orodha kamili ya wanasoka wa kiume walioteuliwa kuwania tuzo hiyo ya kifahari:-

  1. Jude Bellingham -  Real Madrid/England
  2. Ruben Dias -  Man City/Portugal
  3. Phil Foden -  Man City/England
  4. Federico Valverde -  Real Madrid/Uruguay
  5. Emiliano Martinez -  Aston Villa/Argentina
  6. Erling Haaland -  Man City/Norway
  7. Nico Williams - Athletic Club/Spain
  8. Granit Xhaka - Bayer Leverkusen/Switzerland
  9. Artem Dovbyk - Girona/Roma/Ukraine
  10. Toni Kroos - Real Madrid/Germany
  11. Vinicius Junior - Real Madrid/Brazil
  12. Dani Olmo - RB Leipzig/Barcelona/Spain
  13. Florian Wirtz - Bayer Leverkusen/Germany
  14. Martin Odegaard - Arsenal/Norway
  15. Mats Hummels - Borussia Dortmund/Roma/Germany
  16. Rodri - Man City/Spain
  17. Harry Kane - Bayern Munich/England
  18. Declan Rice- Arsenal/England
  19. Vitinha - PSG/Portugal
  20. Cole Palmer - Chelsea/England
  21. Dani Carvajal - Real Madrid/Spain
  22. Lamine Yamal - Barcelona/Spain
  23. Bukayo Saka - Arsenal/England
  24. Hakan Calhanoglu - Inter/Turkey
  25. William Saliba - Arsenal/France
  26. Kylian Mbappe - PSG/Real Madrid/France
  27. Lautaro Martinez - Inter/Argentina
  28. Ademola Lookman - Atalanta/Nigeria
  29. Antonio Rudiger - Real Madrid/Germany
  30. Alejandro Grimaldo - Bayer Leverkusen/Spain