logo

NOW ON AIR

Listen in Live

(VIDEO) Mchezaji amshinda mwenzake, apewa hongera ya kofi kali kuliko lile la Will Smith kwa Chris Rock

Raphael Ankrah awa Ghana alimshinda mwenzake Mfaransa Michael Kouame, na Kouame akampongeza kwa kofi

image
na Radio Jambo

Yanayojiri08 April 2022 - 07:28

Muhtasari


• Runinga ya Fox iliripoti kwamba mchezaji huyo wa Ufaransa alichukizwa na uhalisia kwamba mchezaji wa Ghana ambaye ni mdogo kiumri alimshinda katika mchezo huo wa tenisi.

Michael Kouame akimpiga kofi Raphael Ankrah

Katika video moja ambayo imesambazwa pakubwa kwenye mtandao wa Instagram, inaonesha mchezaji mmoja wa tenisi akimzaba kofi moto mchezaji mwingine aliyemshinda katika mchezo huo.

Katika kile kinaonekana kaam maigizo ya kitendo cha muigizaji Will Smith akimzaba kofi mchekeshaji Chris Rock kwa kumdhihaki mkewe katika hafla ya tuzo za Oscars wiki mbili zilizopita, mchezaji huyo wa Ufaransa, Michael Kouame anamkaribia mwenzake wa Ghana Raphael Ankrah na kumzaba kofi la kushtukiza.

Runinga ya Fox iliripoti kwamba mchezaji huyo wa Ufaransa alichukizwa na uhalisia kwamba mchezaji wa Ghana ambaye ni mdogo kiumri alimshinda katika mchezo huo wa tenisi na kumuita kama vile anataka kumpa hongera lakini hongera yenyewe ikawa kofi la moto wa tanuru.

Mashindano hayo ya kimataifa ya mchezo wa tenisi yalikuwa yanafanyika katika mji mkuu wa Ghana ambapo baada ya mwenyeji kumchachafya mgeni katika raudni ya kwanza, mgeni alikosa heshima na kujiliwaza na kumzaba kofi mwenyeji wake.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved